Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Ikiwa ungeombwa uchague mtawala wa ulimwengu, ungechagua nani? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia sifa za kustahili za Masihi, yule ambaye Mungu amechagua atiawale dunia. Pia linaeleza yale ambayo utawala wake utawafanyia wanadamu.” Soma Isaya 9:6, 7.
Amkeni! Feb.
“Watu huabudu miungu mingi sana leo. Hata hivyo, ona kile ambacho Yesu alisema aliposali kwa Baba yake wa mbinguni. [Soma Yohana 17:3.] Ikiwa kuna Mungu mmoja tu wa kweli, basi tunapaswa kuionaje miungu mingine yote? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia maoni ya Biblia.” Onyesha makala kwenye ukurasa wa 28-29.
Mnara wa Mlinzi Mar. 1
“Watu wengi hukubali kwamba tunapaswa kupendana kama vile Yesu alivyoamuru katika andiko hili. [Soma Yohana 13:34, 35.] Lakini tunaweza kuwapata wapi watu wanaofuata mafundisho ya Yesu maishani mwao? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ambavyo tunaweza kuwatambua Wakristo wa kweli leo.”
Amkeni! Mar.
“Upendo ni muhimu ili tuwe na furaha na maisha mazuri. Hata hivyo, ni vigumu kwa watu wengi kupata upendo wa kweli. Unafikiri kwa nini iko hivyo? [Mruhusu ajibu.] Siri moja ya kupata upendo wa kweli ni kujifunza kuwaonyesha wengine upendo usio na ubinafsi. Gazeti hili linazungumzia jinsi unavyoweza kufanya hivyo.” Soma 1 Wakorintho 13:4-7.