Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Katika miaka ya karibuni, watu wamekuwa wakipendezwa sana na malaika. Je, umewahi kujiuliza malaika ni nani na wanaathirije maisha yetu? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Zaburi 34:7.] Gazeti hili linazungumzia yale ambayo Biblia husema kuhusu mambo ambayo malaika walifanya zamani, wanayofanya sasa, na watakayofanya wakati ujao.”
Amkeni! Jan.
“Leo kuna mashauri kuhusu karibu kila jambo. Ni mashauri gani tunayoweza kutumainia? [Mruhusu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16.] Toleo hili la Amkeni! linaonyesha jinsi tunavyoweza kuitegemea Biblia kuwa chanzo cha mwongozo wenye kutegemeka wa hekima inayotumika.” Mwonyeshe makala kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Sote tunahitaji pesa ili kuendelea kuishi. Lakini je, hukubali kwamba kuna uhitaji wa kujilinda dhidi ya hatari inayotajwa hapa? [Soma 1 Timotheo 6:10, na umruhusu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linatusaidia kutambua baadhi ya mitego ya ufanisi wa kimwili na linaeleza jinsi tunavyoweza kuiepuka.”
Amkeni! Feb.
“Wengi wetu ambao tuna watu wa ukoo na marafiki waliozeeka hujiuliza tunaweza kuwasaidiaje wakabiliane na uzee. Sivyo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linataja mambo tunayoweza kufanya ili kukabiliana na matatizo ya uzee. Pia linaeleza jinsi unabii huu utakavyotimizwa.” Soma Ayubu 33:25.