Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Unafikiri wenzi wa ndoa wanaweza kupata wapi ushauri unaofaa? [Mruhusu ajibu.] Ona ni nani aliyeanzisha ndoa. [Soma Mwanzo 2:22.] Mungu pia alitoa maelekezo yanayofaa kuhusu daraka la mume na la mke. Gazeti hili linaeleza kuhusu mambo hayo.”
Amkeni! Jan.
“Je, umegundua kwamba wengi wanaodai kuwa Wakristo hawafuati mafundisho ya Yesu? [Mruhusu ajibu.] Kwa mfano, wengi hawafuati maneno haya ya Yesu. [Soma Yohana 13:35.] Gazeti hili linazungumzia tofauti kati ya kile ambacho Yesu alifundisha na maoni ya wengi wanaodai kuwa Wakristo.” Mwonyeshe makala inayoanza ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Je, unafikiri kwamba eneo letu lingekuwa mahali bora ikiwa kila mtu angeishi kulingana na maneno haya? [Soma Waefeso 4:25. Kisha mruhusu ajibu.] Watu wengi wanafikiri kwamba kudanganya ni sawa katika hali fulani. Gazeti hili linaelezea faida ya kusema kweli nyakati zote.”
Amkeni Feb.
“Katika jumuiya fulani mtazamo wa watu kuelekea dini umebadilika. Je, unafikiri kwamba dini haziwavutii watu tena? [Mruhusu ajibu.] Maneno haya ya mtume Paulo yanaonyesha sababu kwa nini watu wengi wamepoteza tumaini kuelekea dini. [Soma Matendo 20:29, 30.] Gazeti hili linaonyesha kile ambacho Biblia inasema kuhusu wakati ujao wa Ukristo.”