Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Kwa sababu ya umwagikaji mwingi wa damu ambao umetokea, wafikiri uovu umeshinda wema? [Ngoja jibu.] Ona vile Biblia inavyosema kumhusu Mungu. [Soma Zaburi 83:18b.] Kwa kuwa Mungu ndiye Aliye Juu Zaidi ya dunia yote, je, kweli uovu waweza kushinda? [Ngoja jibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi latupatia jibu lenye kuridhisha la swali hilo.”
Amkeni! Jan. 22
“Usalama wetu unatishwa sana wakati huu kuliko wakati mwingine wowote. Hasa jambo lenye kuhangaisha ni jinsi watu wanavyoweza kutumia jina letu vibaya ili kulaghai. Je, umepata kusikia jambo hilo? [Ngoja jibu.] Biblia inaahidi kwamba siku moja dunia hii haitakuwa tena na ukosefu wa usalama. [Soma Isaya 11:9.] Gazeti hili laeleza jinsi jambo hilo litakavyotimizwa.”
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Leo watu wengi wana wasiwasi kuhusu ukosefu wa kazi, na wengine wana mkazo mwingi sana kazini. Je, wafikiri inawezekana kuwa na furaha na kuhisi salama kazini? [Ngoja jibu. Kisha soma Isaya 65:21-23.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi lazungumzia wakati ambapo watu wote watakuwa na kazi yenye kuridhisha.”
Amkeni! Feb. 8
“Toleo hili la Amkeni! laripoti jambo moja lenye kusikitisha sana katika nyakati zetu—ukahaba wa watoto. Biblia inaahidi kwamba tendo hilo katili litakoma hivi karibuni. [Soma Mithali 2:21, 22.] Gazeti hili laonyesha kile kinachosababisha tatizo hilo na jinsi litakavyokomeshwa.”