Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Kuna wasiwasi mwingi sana kuhusu uchafuzi wa mazingira. Lakini umewahi kufikiria juu ya uchafuzi wa akili? [Ngoja ajibu.] Biblia hukazia umuhimu wa kuwa safi kimwili na kiroho. [Soma 2 Wakorintho 7:1.] Nina hakika kwamba habari hii itakufaa na itakusaidia.”
Amkeni! Feb. 8
“Bila shaka umeona kwamba ijapokuwa ndoa huanza kwa shangwe, nyingi huvunjika. Ningependa kukuachia gazeti hili la Amkeni!, kwa kuwa lazungumzia maoni ya Biblia kuhusu jinsi ya kufanya ndoa idumu na iwe yenye furaha.”
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Je, umepata kujiuliza jinsi unavyoweza kuongoza maisha yako vizuri na kufikia maamuzi muhimu? [Ngoja ajibu.] Biblia hutoa miongozo bora, kama vile ile Kanuni Bora. [Soma Mathayo 7:12.] Ni kanuni gani nyingine za Mungu zinazoweza kutunufaisha moja kwa moja? Utapata jibu katika gazeti hili.”
Amkeni! Feb. 22
“Labda umegundua kwamba siku hizi kumekuwa na hatari nyingi sana kazini. Gazeti hili lina madokezo mazuri ya jinsi tunavyoweza kuwa salama kazini. Pia laonyesha kwamba hali yetu njema inategemea kama tuna maoni yanayofaa kuhusu kazi. Tafadhali lisome.”