Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Kwa sababu ahadi huvunjwa sana siku hizi, wengi huona ni vigumu kumtumaini mtu yeyote. Je, unafikiri kuna yeyote ambaye tunaweza kuamini ahadi zake? [Ngoja jibu. Kisha usome Yoshua 23:14.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kuzitumaini ahadi za Mungu zilizoandikwa katika Biblia.”
Amkeni! Jan. 22
“Hili ndilo jina la Mungu katika lugha ya Kiebrania. [Onyesha jalada.] Watu fulani wanaamini kwamba jina hili halipaswi kutamkwa. Wengine hulitumia kwa uhuru. Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia maoni hayo tofauti. Pia linazungumzia jinsi tunavyoweza kujua jina la Mungu.” Soma Zaburi 83:18.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Wengi wetu hujaribu kutunza afya yetu. Hata hivyo, uchunguzi wa hivi karibuni unaonyesha kwamba hali yetu ya kiroho pia huathiri afya yetu. Je, unafikiri jambo hilo linawezekana? [Ngoja jibu. Kisha usome Mathayo 5:3.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi tunavyoweza kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho.”
Amkeni! Feb. 8
“Watu wengi leo wana maisha yenye shughuli nyingi nao wanahitaji kupumzika zaidi. Labda unakubaliana na maneno haya yaliyoandikwa zaidi ya miaka 3,000 iliyopita. [Soma Mhubiri 4:6. Kisha ngoja jibu.] Gazeti hili la Amkeni! lina habari yenye msaada kuhusu jinsi ya kutambua na kukabiliana na tatizo la deni la usingizi.”