Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Sote tunatamani kuishi maisha bora pamoja na watoto wetu, lakini wengi huhisi kwamba hawana uwezo huo. Je, unafikiri tuna uwezo wa kuamua jinsi wakati wetu ujao utakavyokuwa? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linaonyesha kwamba kulingana na Biblia tuna uwezo huo, kwa kuwa wakati wetu ujao unategemea maamuzi tunayofanya sasa.” Soma Kumbukumbu la Torati 30:19.
Amkeni! Jan. 22
“Tunapokuwa na matatizo ya afya, sisi sote huthamini daktari anayejali hisia zetu. Lakini, je, unafikiri wagonjwa wengi hujali hisia za daktari? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia matatizo ambayo madaktari hukabili na jinsi matibabu yatakavyokuwa wakati ujao.” Soma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
Je, wewe hufadhaika unapoona kwamba watu wengi leo hutendewa jeuri na kukandamizwa? [Taja jambo ambalo limetukia karibuni linalojulikana katika eneo lenu, na ungojee jibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyouona uhai wa mwanadamu. Linaeleza pia jinsi atakavyowakomboa wanadamu kutoka katika mateso yanayowapata leo.” Soma Zaburi 72:12-14.
Amkeni! Feb. 8
“Kuwa na mfadhaiko ni mojawapo ya matatizo makubwa tunayokabili leo. Sivyo? [Ngojea jibu.] Biblia ilitabiri kwa usahihi kwamba hali ingekuwa hivyo. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yanayoweza kukusaidia wewe na familia yako kukabiliana na mfadhaiko.”