Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Watu fulani wanasema kwamba mwanadamu anaiharibu dunia. Je, jambo hilo linakuhangaisha? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii yenye kutia moyo. [Soma Ufunuo 11:18.] Gazeti hili linazungumzia mambo yanayofanya dunia iwe ya pekee. Pia, linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu wakati ujao wa dunia.”
Amkeni! Feb.
“Unafikiri hii ndiyo sababu kuna matatizo mengi sana ulimwenguni? [Soma 1 Yohana 5:19. Kisha mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kumhusu ‘yule mwovu’ na jinsi tunavyoweza kuepuka uvutano wake wenye nguvu.” Mwonyeshe makala inayoanza katika ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Watu wengi wanasema kwamba dini zote zinawaongoza watu kwa Mungu. Je, unafikiri ni sawa kuchagua dini yoyote ile? [Mruhusu ajibu.] Ona pendekezo linalotolewa hapa. [Soma 1 Yohana 4:1.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kuyajaribu mafundisho ili kuona kama yanatokana na Mungu. Pia, linaeleza jinsi dini zilivyoanza.”
Amkeni Mac.
“Unafikiri ni matatizo gani ambayo vijana wanakabili leo? [Mruhusu ajibu.] Mstari huu unazungumzia tatizo moja, yaani, kupata marafiki wazuri. [Soma Methali 13:20.] Gazeti hili linaeleza hatari za kutumia Intaneti kutafuta marafiki na jinsi vijana wanavyoweza kulindwa.”