Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Watu wengi wanahangaishwa na mambo mabaya ambayo yamefanywa katika jina la dini. Wengine wanahisi kwamba dini ndiyo chanzo cha matatizo ya wanadamu. Je, umewahi kufikiria jambo hili? [Ngoja jibu. Kisha usome Ufunuo 18:24.] Gazeti hili linaonyesha maoni ya Biblia kuhusu jambo hilo.”
Amkeni! Feb. 22
“Watu wengi hufurahia kujifunza kuhusu wanyama, na baadhi yao hupenda kuwa na wanyama-vipenzi. [Ngoja maelezo.] Gazeti hili linazungumzia baadhi ya matatizo ya kuwa na wanyama-vipenzi. Pia linaeleza ahadi ya Mungu kuhusu wakati ambapo wanyama wote wataishi kwa amani pamoja na wanadamu.” Soma Isaya 11:6-9.
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Pindi moja, Yesu Kristo aliulizwa hivi: ‘Ni amri gani iliyo ya kwanza kati ya zote?’ Ona jibu lake. [Soma Marko 12:29, 30.] Unafikiri Yesu alimaanisha nini? [Ngoja jibu.] Makala hii, ‘Jinsi Tunavyoonyesha Tunampenda Mungu’ inaeleza maana ya maneno hayo yanayojulikana sana.”
Amkeni! Mac. 8
“Zamani watu wengi waliogopa vita vya nyuklia. Unafikiri vita vya nyuklia vinaweza kuzuka leo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia matukio ya hivi karibuni yanayotuhusu sisi sote. Linaeleza pia ahadi ya Biblia ya ulimwengu ambamo watu hawataishi kwa woga.” Soma Sefania 3:13.