Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Mara kwa mara tunasikia habari kwamba mwujiza umetukia. [Taja kisa kimoja.] Watu fulani hutilia shaka habari hizo, na wengine huziamini. Gazeti hili linazungumzia kama tunaweza kuwa na hakika kwamba miujiza inayotajwa katika Biblia ilitukia, na kama miujiza hutukia leo.” Soma Yeremia 32:21.
Amkeni! Feb. 22
“Zamani za kale, Mungu aliwaamuru watoto waheshimu mama na baba. [Soma Kutoka 20:12.] Je, unafikiri kwamba akina mama wanaheshimiwa ifaavyo leo? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia magumu ambayo akina mama katika nchi mbalimbali wanakabili na jinsi wanavyopambana na magumu hayo.”
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Je, unafikiri kwamba hali ya ulimwengu ingekuwa bora ikiwa watu wangefuata ushauri huu? [Soma Waroma 12:17, 18, kisha ngojea jibu.] Jambo la kusikitisha ni kwamba kutoelewana hutokea mara kwa mara. Gazeti hili linaonyesha jinsi ushauri wa Biblia unavyoweza kutusaidia kusuluhisha ugomvi na kufanya amani.”
Amkeni! Mac. 8
“Uhitaji wa nishati huongezeka kila mwaka. Je, unaweza kuwazia jinsi ambavyo hali ingekuwa ikiwa vyanzo vya nishati kama vile petroli vingeisha? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia maendeleo ambayo yamefanywa ili kupata nishati bila kuchafua mazingira. Linazungumzia pia yule ambaye ni chanzo cha nishati yote.” Soma Isaya 40:26.