Sanduku La Swali
Kuna manufaa gani za kuhudhuria mikutano katika kutaniko la eneo tunamoishi?
Sisi hupokea kitia-moyo cha ‘kutuchochea kwenye upendo na kazi zilizo bora’ kupitia kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Kupitia kutaniko, twajifunza kweli na twatayarishwa ili kutimiza mgao wetu wa kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Pia twaimarishwa kuvumilia majaribu kwa uaminifu na tuna waangalizi wenye upendo wanaotusaidia tukabiliane na mikazo na mahangaiko yanayozidi kuongezeka. Ni wazi kwamba kutaniko hutusaidia kuendelea kiroho. Hata hivyo, je, kuna manufaa za kuhudhuria mikutano katika kutaniko la eneo tunamoishi?
Hali za watu mmoja-mmoja zinatofautiana, na mambo kama vile kazi, mwenzi asiyeamini, na usafiri yanaweza kuhusika mtu anapofanya uamuzi kuhusiana na jambo hilo. Lakini, kwa kweli kuna manufaa za kiroho na faida nyinginezo mtu anaposhirikiana na kutaniko la eneo anamoishi. Wazee wanaweza kuwafikia wahubiri wote kwa uharaka zaidi hali ya dharura itokeapo. Masanduku ya Maswali ya miaka iliyopita yamekazia manufaa kadhaa nyingine.—Mei 1991, Aprili 1976, na Januari 1967 (Kiingereza).
Tunaweza kunufaika zaidi tukihudhuria mikutano iliyo karibu nasi, kwa kuwa hilo hutuwezesha kufika mapema ili tuongee na wengine, kushughulikia mambo ya maana, na kushiriki wimbo na sala ya kufungua. Ikiwa kuna watu wanaopendezwa katika ujirani wetu, mara nyingi tutaweza kuwafikia kwa urahisi, kuongoza mafunzo ya Biblia, na kuwaelekeza kwenye mikutano iliyo karibu nao.
Tuna uhakika kwamba vichwa vya familia watasali kuhusu jambo hilo na kufikiria kwa uzito mambo yote yanayohusika ili waamue jambo litakalofaa familia zao kiroho na kimwili.—1 Tim. 5:8.