Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/02 uku. 7
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Twahitaji Kutaniko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kundi la Kikristo na Utendaji Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 11/02 uku. 7

Sanduku La Swali

Kuna manufaa gani za kuhudhuria mikutano katika kutaniko la eneo tunamoishi?

Sisi hupokea kitia-moyo cha ‘kutuchochea kwenye upendo na kazi zilizo bora’ kupitia kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Kupitia kutaniko, twajifunza kweli na twatayarishwa ili kutimiza mgao wetu wa kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Pia twaimarishwa kuvumilia majaribu kwa uaminifu na tuna waangalizi wenye upendo wanaotusaidia tukabiliane na mikazo na mahangaiko yanayozidi kuongezeka. Ni wazi kwamba kutaniko hutusaidia kuendelea kiroho. Hata hivyo, je, kuna manufaa za kuhudhuria mikutano katika kutaniko la eneo tunamoishi?

Hali za watu mmoja-mmoja zinatofautiana, na mambo kama vile kazi, mwenzi asiyeamini, na usafiri yanaweza kuhusika mtu anapofanya uamuzi kuhusiana na jambo hilo. Lakini, kwa kweli kuna manufaa za kiroho na faida nyinginezo mtu anaposhirikiana na kutaniko la eneo anamoishi. Wazee wanaweza kuwafikia wahubiri wote kwa uharaka zaidi hali ya dharura itokeapo. Masanduku ya Maswali ya miaka iliyopita yamekazia manufaa kadhaa nyingine.—Mei 1991, Aprili 1976, na Januari 1967 (Kiingereza).

Tunaweza kunufaika zaidi tukihudhuria mikutano iliyo karibu nasi, kwa kuwa hilo hutuwezesha kufika mapema ili tuongee na wengine, kushughulikia mambo ya maana, na kushiriki wimbo na sala ya kufungua. Ikiwa kuna watu wanaopendezwa katika ujirani wetu, mara nyingi tutaweza kuwafikia kwa urahisi, kuongoza mafunzo ya Biblia, na kuwaelekeza kwenye mikutano iliyo karibu nao.

Tuna uhakika kwamba vichwa vya familia watasali kuhusu jambo hilo na kufikiria kwa uzito mambo yote yanayohusika ili waamue jambo litakalofaa familia zao kiroho na kimwili.—1 Tim. 5:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki