Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/91 uku. 3
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Mahubiri ya Vikundi Huleta Shangwe
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kutaniko na Lijengwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 5/91 uku. 3

Sanduku la Swali

Kwa nini inapendekezwa kwamba wahubiri watumike pamoja na kundi lenye eneo ambamo wanaishi?

Ni jambo la maana kufanya mambo kwa njia yenye utaratibu na ya kitheokrasi. Mtume Paulo aliandika: “Kwa mana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani. . . . Mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”—1 Kor. 14:33, 40.

Ingawa huenda kukawa na tofauti fulani kwa sababu ya magumu ya usafiri, ratiba za kazi ya kuajiriwa, au uhitaji wa usaidizi katika uangalizi, kwa kawaida yafaa zaidi kuhudhuria kundi ambalo twaishi katika eneo lalo. Hiyo hufanya ifae zaidi kwa utumishi wa shambani, na sisi hatuhitaji kusafiri mbali sana kufanya kazi pamoja na kikundi nje ya ujirani wetu. Inatuweka katika hali bora zaidi ya kufanya kazi pamoja na wengine katika kundi letu na kuwaelekeza wapya wenye kupendezwa kwenye mikutano panapowafaa zaidi. Na inatuweka katika hali ya kuweza kuwasiliana kwa urahisi zaidi na akina ndugu na dada wengine katika eneo letu ambao waweza kutusaidida wakati wa uhitaji.

Kwa kufanya kazi kwa ujitiisho katika mipango iliyofanywa, sisi twaonyesha kwamba twatanguliza masilahi ya Ufalme. (Luka 16:10) Kundi jipya linapofanyizwa au Mafunzo ya Kitabu ya Kundi yanapopangwa upya, huenda tukapendelea zaidi kukaa pamoja na marafiki fulani. Lakini kwa kukubali huo mpango mpya, twaweza kupata marafiki wapya na kupanua zaidi mashirika yetu ya kitheokrasi. Pia, huwa ni rahisi zaidi kwa wazee kuchunga kundi na kufanyia maendeleo hali ya kiroho ya kundi ikiwa wahubiri wanaishi ndani ya eneo la kundi wanaloshirikiana nalo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki