Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/03 uku. 1
  • ‘Kung’aa Tukiwa Wamulikaji’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kung’aa Tukiwa Wamulikaji’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Vijana Wanaoangaza Kama Mianga
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Kuacha Nuru Yetu Ing’ae kwa Uendelevu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • “Acheni Nuru Yenu Ing’ae”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • “Kuwa Kama Mianga Katika Ulimwengu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 4/03 uku. 1

‘Kung’aa Tukiwa Wamulikaji’

1 Waabudu wapatao milioni sita wa Mungu wa kweli Yehova, ‘wanang’aa wakiwa wamulikaji’ katika nchi 234 katika ulimwengu wenye giza la kiroho na hali mbaya za kimaadili. (Flp. 2:15) Hilo hutufanya tuwe tofauti. Tuonyesheje nuru ya kweli yenye thamani ambayo hutoka kwa Yehova?—2 Kor. 3:18.

2 Matendo Yetu: Watu huwa wepesi kuona mwenendo wetu. (1 Pet. 2:12) Mwanamke mmoja alisema kwamba mfanyakazi mwenzake aliye Shahidi alikuwa mwenye fadhili na tayari kusaidia wala hakutumia lugha chafu au kufurahia mizaha michafu. Wengine walipojaribu kumchokoza Shahidi huyo kwa kuongea mambo machafu, alibaki mtulivu na kushikilia lililo sawa. Mwenendo wake ulikuwa na matokeo gani kwa mwanamke huyo? Anasema hivi: “Nilivutiwa sana na mwenendo wake nikaanza kumwuliza maswali kuhusu Biblia. Nilianza kujifunza Neno la Mungu na baadaye nikabatizwa.” Aongezea hivi: “Ni mwenendo wake ulionifanya nichunguze mafundisho ya Mashahidi wa Yehova.”

3 Mtazamo wetu kuelekea wenye mamlaka, maoni yetu kuhusu matendo ya kilimwengu, na usemi wetu mzuri hufanya Mashahidi wa Yehova wajulikane kuwa watu wanaoishi kupatana na viwango vya juu vya Biblia. Matendo hayo mazuri yanaweza kumtukuza Yehova na kuvutia wengine waje kumwabudu.

4 Maneno Yetu: Kwa kweli, wale wanaoona mwenendo wetu mzuri huenda wasijue sababu inayotufanya tuwe tofauti tusipowahubiria. Je, wafanyakazi au wanashule wenzako wanajua kwamba wewe ni Shahidi wa Yehova? Je, wewe hutafuta fursa za kutoa ushahidi katika maongezi ya kawaida? Je, umeazimia ‘kuacha nuru yako ing’ae mbele ya watu’ wakati wowote unaofaa?—Mt. 5:14-16.

5 Ni lazima tuwe na roho ya kujidhabihu ili tutimize kazi yetu tukiwa wamulikaji. Nia ya kutumikia kwa nafsi yote itatuchochea kujinyima mambo yasiyo muhimu ili tufanye mengi kadiri tuwezavyo katika kazi ya kuokoa uhai ya kuhubiri na kufanya wanafunzi.—2 Kor. 12:15.

6 Na twendelee kung’aa tukiwa wamulikaji kwa maneno na matendo yetu. Tukifanya hivyo, wengine wanaweza kujiunga nasi ili kumtukuza Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki