Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/03 uku. 1
  • Pongezi Hutia Moyo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pongezi Hutia Moyo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • “Neno Linalosemwa Wakati Unaofaa Ni Jema Kama Nini!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Tambua Umuhimu wa Kutoa Pongezi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kuwapongeza
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Kwa Nini Uwapongeze Wengine?
    Amkeni!—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 11/03 uku. 1

Pongezi Hutia Moyo

1 “Je, sijawa mtoto mzuri leo?” Hivyo ndivyo msichana mdogo alivyouliza huku machozi yakimtiririka wakati wa kulala. Swali hilo lilimshangaza mamake. Ijapokuwa aliona jinsi msichana wake mdogo alivyojitahidi sana kuwa na adabu siku hiyo, alikosa kumpongeza. Machozi ya msichana huyo mdogo yanapaswa kutukumbusha kwamba sisi sote tunahitaji pongezi, tuwe wachanga au wakubwa. Je, sisi huwatia moyo wengine kwa kuwapongeza kwa sababu ya mambo mazuri wanayofanya?—Met. 25:11.

2 Tuna sababu nyingi nzuri za kuwapongeza Wakristo wenzetu. Wazee, watumishi wa huduma, na mapainia hujitahidi sana kutimiza madaraka yao. (1 Tim. 4:10; 5:17) Wazazi wanaomwogopa Mungu hujitahidi kadiri wawezavyo kuwalea watoto wao kupatana na njia za Yehova. (Efe. 6:4) Vijana Wakristo wanajikakamua sana kuipinga “roho ya ulimwengu.” (1 Kor. 2:12; Efe. 2:1-3) Wengine humtumikia Yehova kwa uaminifu licha ya uzee, matatizo ya afya, au magumu mengine. (2 Kor. 12:7) Wote hao wanastahili pongezi. Je, sisi huwapongeza kwa sababu ya jitihada zao?

3 Toa Pongezi Hususa kwa Mtu Binafsi: Kwa kweli sisi sote hufurahi kutaniko lote linapopongezwa. Hata hivyo, tunatiwa moyo zaidi tunapopongezwa kibinafsi. Kwa mfano, katika sura ya 16 ya barua yake kwa Waroma, Paulo aliwapongeza kihususa, Fibi, Priska, Akila, Trifaina, Trifosa, Persisi, na wengineo. (Rom. 16:1-4, 12) Bila shaka maneno yake yaliwatia moyo kwelikweli waaminifu hao! Kuwasifu ndugu na dada zetu kwa njia hiyo huwahakikishia kwamba wanahitajiwa na huboresha uhusiano wetu. Je, umempongeza kihususa mtu fulani hivi karibuni?—Efe. 4:29.

4 Kutoka Moyoni: Ili tuwatie wengine moyo kwelikweli, lazima tuwapongeze kutoka moyoni. Watu wanaweza kujua kama tunaongea kutoka moyoni au ikiwa ‘tunawabembeleza tu kwa ulimi.’ (Met. 28:23) Tunapojizoeza kuona sifa nzuri za wengine, moyo wetu utatuchochea kuwapongeza. Na tuwapongeze wengine sana kutoka moyoni tukijua kwamba “neno linalosemwa wakati unaofaa ni jema kama nini!”—Met. 15:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki