Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/04 uku. 4
  • Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1990
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1996
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 6/04 uku. 4

Chakula cha Kiroho kwa Wakati Unaofaa

1 ‘Nitaiita nafaka na kuifanya iwe tele, nami sitaweka juu yenu njaa yoyote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. (Eze. 36:29) Maneno hayo ya kinabii yanawahusu watu wa Mungu leo. Kwa njia ya mfano, Yehova amewachipushia watu wake kwa wingi nafaka zinazotegemeza uhai. Chakula cha kiroho cha wakati unaofaa kinachoandaliwa katika makusanyiko yetu ya wilaya  kinathibitisha jambo hilo.

2 Katika kusanyiko lililofanywa Columbus, Ohio, mwaka wa 1931, Yehova aliwaelekeza waabudu wake wajipatie jina jipya—Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10-12) Katika mwaka wa 1935 umati mkubwa unaotajwa kwenye Ufunuo 7:9-17 ulitambuliwa kwa usahihi. Mwaka wa 1942, ndugu Knorr alitoa hotuba yenye kichwa “Amani—Inaweza Kudumu?” Hotuba hiyo ilichochea kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote na ikafanya Shule ya Gileadi (Watchtower Bible School of Gilead) ianzishwe. Ingawa makusanyiko fulani hukumbukwa sana, kila moja limekuwa meza iliyojaa chakula cha kiroho chenye lishe kinachoandaliwa kwa wakati unaofaa.—Zab. 23:5; Mt. 24:45.

3 Je, Wewe Unakula Vema? Ikiwa mtu hafanyi bidii ya kula, anaweza kukosa lishe ya kutosha hata ingawa ana chakula kingi. (Met. 26:15) Ndivyo ilivyo katika hali ya kiroho. Katika makusanyiko machache, imeonekana kwamba watu wengi wanatembea-tembea bila sababu au kuongea na wengine wakati wa programu. Ingawa ushirika wenye kujenga ni sehemu muhimu ya kusanyiko, wakati wa kufanya hivyo ni kabla na baada ya kila kipindi. (Mhu. 3:1, 7) Ikiwa hatutaketi na kusikiliza kwa makini, huenda tukakosa jambo muhimu. Mara kwa mara huenda waangalizi wa idara za kusanyiko na ndugu wengine wenye migawo wakalazimika kuzungumza mambo yanayohusu kusanyiko huku vipindi vikiendelea. Wakati wanapokuwa hawana shughuli hizo, wanapaswa kuweka mfano kwa kusikiliza programu kwa makini. Yeyote kati yetu hapaswi kukosa sehemu yoyote ya chakula hicho cha kiroho tunachoandaliwa.—1 Kor. 10:12; Flp. 2:12.

4 Tunafurahia sana kweli za kiroho ambazo Yehova huandaa, kinyume na mafundisho ya uwongo yasiyojenga ya Jumuiya ya Wakristo! (Isa. 65:13, 14) Njia moja ya ‘kujionyesha kuwa wenye shukrani’ ni kwa kuliona kusanyiko kuwa nafasi ambayo Yehova hutumia kutufundisha. (Kol. 3:15) Usikaze fikira zako kwa msemaji tu bali kwenye hotuba, na uuone ujumbe huo kama unaotoka kwa ‘Mfundishaji wetu Mkuu.’ (Isa. 30:20, 21; 54:13) Sikiliza kwa makini. Andika mambo makuu kwa ufupi. Pitia mambo makuu ya programu kila jioni. Tumia yale unayojifunza.

5 Kila kusanyiko linalofanyika wakati huu kabla ya Har–Magedoni ni ushindi dhidi ya Shetani, iwe linafanywa katika kambi ya wakimbizi, katika nchi zilizo na vita, au katika uwanja mkubwa wenye utulivu. Tukiwa undugu wenye umoja tunathamini nafasi za kukutana pamoja kwenye makusanyiko ya wilaya. (Eze. 36:38) Tuna uhakika kwamba Yehova atatuandalia tena kwa upendo “chakula katika wakati unaofaa.”—Luka 12:42.

[Maswali ya Funzo]

1. Andiko la Ezekieli 36:29 linatimizwaje leo?

2. Yehova ametumiaje makusanyiko ya wilaya ili kuandaa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa?

3. Tunapaswa kufanya nini ili tufaidike na karamu ya kiroho kwenye kusanyiko letu la wilaya?

4. Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa chakula kingi cha kiroho ambacho Yehova huandaa?

5. Tuna sababu gani za kufurahia makusanyiko ya wilaya?

[Picha katika ukurasa wa 4]

Thamini Meza ya Yehova

◼ Sikiliza kwa makini

◼ Andika mambo makuu

◼ Pitia mambo makuu ya programu kila jioni

◼ Tumia yale unayojifunza

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki