Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/04 uku. 3
  • “Na Tulikweze Jina Lake Pamoja”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Na Tulikweze Jina Lake Pamoja”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Pindi ya Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kukusanyika Ili Tumsifu Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 6/04 uku. 3

“Na Tulikweze Jina Lake Pamoja”

1 “Mtukuzeni Yehova pamoja nami, na tulikweze jina lake pamoja,” akaimba mtunga-zaburi. (Zab. 34:3) Kusanyiko letu la Wilaya lijalo la “Tembea Pamoja na Mungu” litatupa nafasi ya kulikweza jina la Yehova pamoja na ndugu na dada zetu kutoka makutaniko mengi. Je, umefanya mipango ya mahali pa kulala, usafiri, na kuomba ruhusa kazini? Ni jambo la hekima kushughulikia mambo hayo mapema.—Met. 21:5.

2 Kufika Kusanyikoni: Kuna mambo mengi ya kushughulikia tunapohudhuria kusanyiko. Kuondoka mapema kutatusaidia tukabiliane na mambo yoyote yanayoweza kutuchelewesha na kutatuwezesha kuketi kwa wakati unaofaa ili kushiriki kwa moyo wote wimbo na sala ya kufungua. (Zab. 69:30) Mwenyekiti atakuwa ameketi jukwaani dakika chache kabla ya kipindi kuanza huku muziki wa Ufalme ukiendelea. Sisi sote tunapaswa kuwa tumeketi wakati huo ili programu ianze kwa njia ya heshima.—1 Kor. 14:33, 40.

3 Neno la Mungu linatusihi kwamba ‘mambo yetu yote yatendeke kwa upendo.’ (1 Kor. 16:14) Milango inapofunguliwa saa mbili asubuhi, kuwajali wengine kutatuzuia kukimbia, kusukumana, au kupigana vikumbo ili kung’ang’ania viti tunavyopenda kabla ya wengine. Unaweza kuhifadhi viti kwa ajili ya wale tu unaosafiri pamoja nao katika gari moja au wale mnaoishi nao katika nyumba moja.—1 Kor. 13:5; Flp. 2:4.

4 Tafadhali beba chakula cha mchana badala ya kuondoka kusanyikoni ili kwenda kutafuta chakula wakati wa pumziko la mchana. Kufanya hivyo kutawawezesha wote wafurahie ushirika wenye kujenga na kuwapo kipindi cha alasiri kinapoanza. Vyombo vikubwa sana vya kuwekea chakula, vyombo vya glasi, na vileo haviruhusiwi kusanyikoni.

5 Wale wenye matatizo ya kusikia wanapaswa kuwajulisha mapema wasimamizi wa kusanyiko ili wafanyiwe mipango ya kuketi mahali panapofaa.

6 Karamu ya Kiroho Inatungoja: Mfalme Yehoshafati ‘aliutayarisha moyo wake kumtafuta Mungu wa kweli.’ (2 Nya. 19:3) Tunawezaje kuutayarisha moyo wetu kabla ya kusanyiko? Makala zilizo kwenye kurasa za nyuma za magazeti ya Amkeni! ya Mei 22 na Juni 8 zina habari fupi za karamu ya kiroho itakayoandaliwa. Kwa nini usitenge wakati wa kusoma makala hizo, ukiongeza hamu yako kwa ajili ya yale ambayo Yehova ametuwekea akiba? Pia kutayarisha moyo wetu hutia ndani kumwomba Yehova atusaidie kupata maana na kutumia mafundisho tutakayopata.—Zab. 25:4, 5.

7 Sote tunatazamia kwa hamu kujifunza mengi kutoka katika Neno la Mungu, huku tukitambua kwamba tunaweza kufikia wokovu kupitia Neno hilo. (1 Pet. 2:2) Hivyo, na tuhudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na Mungu” na ‘tulikweze jina la Yehova pamoja.’—Zab. 34:3.

[Maswali ya Funzo]

1. Tutakuwa na nafasi gani ya kulikweza jina la Mungu pamoja, na tunaweza kufanya matayarisho gani sasa?

2. Kwa nini inafaa kupanga kufika kusanyikoni mapema?

3. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunawajali wengine tunapotafuta viti?

4. Kuna utaratibu gani kwa ajili ya pumziko la mchana, nao una faida gani?

5. Kuna mipango gani kwa wale walio na matatizo ya kusikia?

6. Tunaweza kutayarishaje mioyo yetu kwa ajili ya mafundisho tutakayopata?

7. Hamu yetu ni nini, na kwa nini?

[Picha katika ukurasa wa 3]

Njia za Kulikweza Jina la Mungu

◼ Panga mapema

◼ Waonyeshe wengine upendo

◼ Tayarisha moyo wako

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki