Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Watu fulani hudhani kwamba mambo yote yanayotokea maishani, kutia ndani misiba, ni mapenzi ya Mungu. Wewe una maoni gani kuhusu jambo hilo? [Ngoja jibu.] Watu wengi wanajua sala hii. [Soma Mathayo 6:10b.] Mapenzi ya Mungu kwa ajili ya dunia ni nini, nayo yatatimizwa kikamili lini? Gazeti hili linatupa jibu la Biblia.”
Amkeni! Apr. 22
“Katika ulimwengu wa sasa, watu fulani huhisi hawana tumaini. Je, wewe huhisi hivyo nyakati nyingine? [Ngoja jibu. Kisha soma Waroma 15:4.] Watu wengi wanatambua umuhimu wa kuwa na tumaini. Utafurahia kusoma sababu saba za Kimaandiko za kuwa na tumaini zinazotajwa katika gazeti hili la Amkeni!”
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Ili kuboresha jamii ya binadamu, viongozi fulani wa kidini hujiingiza katika siasa. Hata hivyo, ona yale aliyofanya Yesu watu walipotaka kumfanya mfalme. [Soma Yohana 6:15.] Yesu alikazia fikira jambo ambalo lingewaletea wengine faida za kudumu. Gazeti hili linazungumzia jambo hilo.”
Amkeni! Mei 8
“Watu wengi hupata magumu kazini. Wengine hata hudhulumiwa na wafanyakazi wenzao. Je, unajua kwamba Biblia ina mashauri yanayoweza kutusaidia kukabiliana na magumu hayo? [Ngoja jibu. Kisha soma Methali 15:1.] Gazeti hili lina madokezo mazuri ya jinsi ya kudumisha amani pamoja na wengine kazini.”