Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/04 uku. 3
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Sifu Yah kwa Njia ya Kupata Maandikisho
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutoa Maandikisho kwa Ujasiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 7/04 uku. 3

Sanduku La Swali

◼ Nakala za kibinafsi za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ziagizweje?

Kwa kuwa mpango wa kuandikisha magazeti na kaseti za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ulikomeshwa muda fulani uliopita, wahubiri wote wanapaswa kupata magazeti, kaseti na CD za M3 kupitia kutaniko lao. Hata hivyo, magazeti na kaseti kwa ajili ya vipofu, ambazo hutumwa bila malipo, zinaweza kuandikishwa kwa ajili ya wale wanaostahili. Tafadhali kumbukeni kwamba makutaniko yanaweza kuomba magazeti yaliyo kwenye kaseti au CD za MP3 kwenye fomu ya Maombi ya Kutaniko (M-202). Matoleo ya lugha za kigeni na chapa kubwa pia yanapaswa kuagizwa kwa kutumia fomu hiyo.

Mtu fulani katika eneo lenu akiomba kuletewa magazeti kwa ukawaida, tafadhali hakikisheni mnafanya hivyo haraka ili asikose hata toleo moja. Watu waliotengwa na ushirika wanaweza kuchukua magazeti au vichapo vingine vya matumizi ya kibinafsi kwenye meza ya magazeti na vichapo katika Jumba la Ufalme. Watu waliotengwa na ushirika hawapaswi kutiwa ndani ya mpango wa kuwapelekea watu magazeti kwa ukawaida.

Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ikitoa ombi la maandikisho kwa ajili ya mtu ambaye hawezi kupata magazeti kupitia njia ya kawaida ya kupelekea watu magazeti, mwandishi anapaswa kutia ndani taarifa fupi inayothibitisha kwamba ombi hilo la andikisho limechanganuliwa na kuidhinishwa na Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko.

Hiyo inamaanisha kwamba wahubiri hawapaswi kuandikia ofisi ya tawi ili kuomba maandikisho ya kibinafsi. Wahubiri au watu wanaopendezwa wakitoa maombi hayo ya maandikisho, yatarudishwa kutanikoni.

◼ Mfungwa aliye gerezani anaweza kupataje magazeti yake ya kibinafsi?

Ikiwa kutaniko linalohubiri eneo lililo na gereza linaweza kuwapelekea wafungwa magazeti, basi mfungwa huyo anapaswa kupokea magazeti yake ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kupitia wahubiri wanaotembelea gereza hilo. Ikiwa haiwezekani kufanya hivyo, mfungwa huyo anaweza kuomba maandikisho kwa kuandikia ofisi ya tawi. Tafadhali kumbukeni kwamba wafungwa waliotengwa na ushirika wanaweza kupata magazeti yao kwa njia zilizoelezwa katika fungu hili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki