Elimu Inayoongoza Kwenye Uzima
1 Inapendeza sana kuona macho ya watu yaking’aa wanapoelewa ukweli wa Neno la Mungu! Inaridhisha sana kuwaeleza wengine ujuzi juu ya Mungu na kusudi lake kwa wanadamu. Elimu kama hiyo inaweza kumwongoza mtu apate uzima wa milele.—Yoh. 17:3.
2 Kinachoifanya Iwe Bora: Leo watu huelimishwa kupitia njia nyingi sana na kuhusu mambo mbalimbali. (Mhu. 12:12) Lakini thamani ya ujuzi kama huo haiwezi kulinganishwa na “mambo makuu ya Mungu.” (Mdo. 2:11) Je, elimu inayotolewa ulimwenguni imeweza kuwavuta watu karibu na Muumba na kuwafanya wafahamu kusudi lake? Je, imewasaidia watu waelewe ni nini hutupata tunapokufa au kwa nini watu wanateseka sana? Je, imewapa watu tumaini? Je, imesaidia kuboresha maisha ya familia? La. Tunaweza kupata majibu halisi ya maswali muhimu zaidi maishani kupitia tu elimu inayotoka kwa Mungu.
3 Elimu inayotoka kwa Mungu hutupa maadili bora ambayo hayapatikani kabisa katika ulimwengu leo. Neno la Mungu hung’oa ubaguzi wa rangi, wa kikabila, na wa kitaifa kutoka mioyoni mwa watu wanaokubali na kufuata mafundisho yake. (Ebr. 4:12) Limewachochea watu waache kila aina ya jeuri na ‘kujivika utu mpya.’ (Kol. 3:9-11; Mika 4:1-3) Isitoshe, elimu inayotoka kwa Mungu imewapa mamilioni nguvu za kukabiliana na mazoea na nyutu zisizompendeza Mungu zilizokuwa zimekita mizizi.—1 Kor. 6:9-11.
4 Kwa Nini Ni Muhimu Sasa?: Mfundishaji wetu Mkuu anatutahadharisha kuhusu umuhimu wa nyakati tunamoishi. Hukumu zake za kinabii zina habari za kisasa ambazo lazima zitangazwe duniani pote. (Ufu. 14:6, 7) Kristo anatawala mbinguni, milki ya ulimwengu ya dini bandia itaharibiwa karibuni, na Ufalme wa Mungu unajitayarisha kuharibu serikali zote za kidunia. (Dan. 2:44; Ufu. 11:15; 17:16) Hivyo, watu wanapaswa kufanya haraka wamtambue Mfalme wa Mungu anayetawala, watoke katika Babiloni Mkubwa, na kuliitia jina la Yehova kwa imani. (Zab. 2:11, 12; Rom. 10:13; Ufu. 18:4) Acheni tushiriki kwa ukamili kadiri tuwezavyo kuwapa wengine elimu inayoongoza kwenye uzima.