Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/06 uku. 1
  • Jinsi ya Kudumisha Bidii

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kudumisha Bidii
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • “Wakeni Roho”
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Watu Wenye Juhudi ya Kazi Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Tangaza Habari Njema kwa Hamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kuingiza Sheria ya Mungu ‘Ndani ya Sehemu Zetu za Ndani’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 4/06 uku. 1

Jinsi ya Kudumisha Bidii

1 Huenda bidii ya Apolo katika huduma ikatukumbusha Wakristo wenzetu leo ambao wana bidii sana katika kazi ya kuhubiri. (Mdo. 18:24-28) Hata hivyo, sote tunaonywa hivi: “Msiwe wavivu katika kazi zenu. Wakeni roho.” (Rom. 12:11) Ni nini kinachoweza kutusaidia kuwa wenye bidii kwa ajili ya huduma ya Kikristo, na kudumisha bidii hiyo?

2 Inachochewa na Ujuzi: Baada ya Yesu kuwatokea wanafunzi wake wawili na ‘kuwafasiria mambo yanayomhusu yeye mwenyewe katika Maandiko yote,’ walisema hivi: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akisema nasi barabarani?” (Luka 24:27, 32) Vivyo hivyo, je, mioyo yetu haiwaki kwa msisimuko tunapozidi kulielewa Neno la Mungu? Naam, imani huchochewa na ujuzi. Andiko la Waroma 10:17 linaeleza hivi: “Imani hufuata jambo lililosikiwa.” Mioyo yetu inapojawa na uhakika katika ahadi za Yehova, hatuwezi kujizuia kusema kuhusu mambo ambayo tumejifunza!—Zab. 145:7; Mdo. 4:20.

3 Lakini hatuwezi kutegemea ujuzi ambao tulipata zamani uimarishe upendo wetu kwa Mungu na utusaidie kuendelea kuwa na bidii katika utumishi wake. Ni lazima tuendelee kupanua uelewaji wetu wa kweli na kuzidisha upendo wetu kwa Yehova. Tusipofanya hivyo, pole kwa pole, utumishi wetu kwake utakuwa wa kidesturi tu. (Ufu. 2:4) Neno la Mungu linatuhimiza ‘tuendelee kuongezeka katika ujuzi sahihi wa Mungu.’—Kol. 1:9, 10.

4 Mazoea Yetu ya Kujifunza: Kwa hiyo, tunapaswa kuchunguza mazoea yetu ya kujifunza. Kwa mfano, huenda tukapiga mstari majibu yote katika makala ya funzo la Mnara wa Mlinzi na kutoa majibu sahihi. Lakini je, sisi husoma Maandiko ambayo hayajanukuliwa na kutafakari jinsi tunavyoweza kutumia habari hiyo maishani? Je, sisi hujitahidi kufanya utafiti wa ziada hali zetu zikiruhusu na kutafakari yale ambayo tunajifunza kutokana na usomaji wa Biblia wa kila juma? (Zab. 77:11, 12; Met. 2:1-5) Tunafaidika sana tunapotafakari na kuzama katika Neno la Mungu. (1 Tim. 4:15, 16) Tukijifunza Biblia hivyo kwa undani, tutategemezwa na kutiwa nguvu ili tuwe na “bidii kwa ajili ya kazi njema.”—Tito 2:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki