Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/06 uku. 4
  • Je, Wewe Huulizia Watu Wanaotaka Kujifunza?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Huulizia Watu Wanaotaka Kujifunza?
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuwasaidia Watu Wenye “Mwelekeo Unaofaa” Kuwa Wanafunzi
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 4/06 uku. 4

Je, Wewe Huulizia Watu Wanaotaka Kujifunza?

Ikiwa kwa sasa unaongoza funzo la Biblia, kwa nini usimwulize mwanafunzi ikiwa rafiki zake na watu wa jamaa wangependa kujifunza mafundisho ya Biblia? Mara nyingi, mwanafunzi huyo atataja watu kadhaa. Baada ya kumwomba mwanafunzi huyo ruhusa, unaweza kutaja jina lake unapoenda kuwatembelea watu hao ili kuwauliza kama wangependa kujifunza Biblia. Huenda ukasema, “[Jina la mwanafunzi] amefurahia kujifunza Biblia, na anafikiri kwamba huenda wewe pia ukanufaishwa na programu yetu ya kufundisha watu Biblia bila malipo.” Kisha mwonyeshe kifupi jinsi ambavyo funzo huongozwa ukitumia kitabu Biblia Inafundisha.

Ikiwa una mwanafunzi ambaye anafanya maendeleo, unaweza kumtia moyo awaeleze rafiki zake na washiriki wa familia ambao huenda wakapendezwa, jinsi ambavyo sisi hujifunza Biblia na watu. Anaweza kuwaalika wahudhurie funzo lake. Au ikiwa haiwezekani, anaweza kupanga ukutane nao ili kuwaonyesha jinsi ambavyo funzo huongozwa. Kufanya hivyo kutamtia moyo mwanafunzi aanze kuwaeleza wengine habari anazojifunza kutoka katika Biblia.

Wale ambao wewe huwatembelea kwa ukawaida pia wanaweza kukutajia watu ambao wangependa kujifunza Biblia, hata ikiwa wao wenyewe hawajakubali kujifunza Biblia kwa ukawaida. Unapowaonyesha kitabu Biblia Inafundisha, huenda ukawauliza, “Je, unajua mtu yeyote ambaye angefurahia kupata kitabu hiki?”

Kwa kuzingatia uharaka wa nyakati tunamoishi, tungependa kutumia kila njia kuwasaidia watu wasikie na kukubali habari njema. Je, wewe huulizia watu wanaotaka kujifunza?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki