Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Karibu kila mtu anakubali kwamba siri moja ya kuwa na maisha ya familia yenye furaha ni mawasiliano mazuri, hata hivyo watu wengi huona ni vigumu kuwasiliana vizuri. Unafikiri ni kwa nini? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linatoa madokezo ya kusitawisha mbinu za kuwasiliana.” Soma Yakobo 1:19.
Amkeni! Apr.
“Watu wengi husema kwamba msalaba huwasaidia kumkaribia Mungu zaidi. Hata hivyo, wengine hujiuliza: Je, inafaa kuabudu kifaa kilichotumiwa kumwua Yesu? Je, kweli Yesu alikufa msalabani? Makala kwenye ukurasa wa 12 inachunguza maswali hayo kwa kuyalinganisha na maoni ya Biblia.” Soma Matendo 5:30.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Mamilioni ya watu ulimwenguni wanaathiriwa sana na umaskini. Unadhani wanaweza kusaidiwaje? [Mruhusu ajibu. Kisha soma 1 Petro 2:21.] Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kufuata kielelezo cha Yesu kwa kuwajali maskini.”
Amkeni! Mei
“Je, umewahi kujiuliza kwa nini sisi huzeeka? [Mruhusu ajibu.] Sababu ambayo Biblia hutoa kuhusu kile kinachofanya tuzeeke inaonyesha jinsi ambavyo Mungu amefanya mpango wa kutuwezesha kuishi milele. [Soma Isaya 25:8.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia baadhi ya uchunguzi ambao umefanywa hivi karibuni kuhusu kuzeeka.”