Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/06 uku. 3
  • Mfano Mzuri kwa Vijana na Wazee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mfano Mzuri kwa Vijana na Wazee
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Igeni Imani Yao
  • Kila Mtu Anaweza Kujifunza Kutokana na Video ya Noah—He Walked With God
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 5/06 uku. 3

Mfano Mzuri kwa Vijana na Wazee

Alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu. Alitumia maisha yake kufanya mapenzi ya Yehova. “Alitembea pamoja na Mungu wa kweli” na akabarikiwa kwa kufanya hivyo. Mtu huyo aliitwa Noa, naye ni mfano unaofaa kuigwa na vijana na vilevile wazee. (Mwa. 6:9) Video Noah—He Walked With God itakusaidia kuwazia jinsi maisha ya Noa yalivyokuwa, sababu iliyofanya astahili baraka za Yehova, na jinsi unavyoweza kuiga sifa zake nzuri. Mahali ambapo hakuna video, kuchunguza Mwanzo sura ya 6 hadi 9 kutatutia moyo kuiga mfano mzuri ambao Noa aliwawekea Wakristo wa kweli katika siku hizi za mwisho.

DVD ya Noah ina maswali yafuatayo. Tazama video hiyo, au ikiwa haipatikani katika eneo lenu, soma maandiko yaliyotajwa hapa kuanzia Mwanzo sura ya 6 hadi 9 kisha ujiulize: (1) Malaika fulani walifanya kosa gani, nao Wanefili walikuwa nani? (Mwa. 6:1, 2, 4) (2) Kwa nini watu walikuwa wabaya sana, naye Mungu alihisije kuhusu hilo? (Mwa. 6:4-6) (3) Noa alitofautianaje nao? (Mwa. 6:22) (4) Waovu waliangamizwaje? (Mwa. 6:17) (5) Safina ilikuwa kubwa kadiri gani? (Mwa. 6:15) (6) Noa alifanya nini kingine, nao watu walitendaje? (Mt. 24:38, 39; 2 Pet. 2:5) (7) Ni wanyama wangapi wa kila aina walioingia ndani ya safina? (Mwa. 7:2, 3, 8, 9) (8) Kulinyesha kwa siku ngapi, nayo dunia ilifunikwa na maji kwa muda gani? (Mwa. 7:11, 12; 8:3, 4) (9) Kwa nini Noa na familia yake waliokoka? (Mwa. 6:18, 22; 7:5) (10) Safina ilitua wapi? (Mwa. 8:4) (11) Noa alijuaje kwamba ilikuwa salama kutoka kwenye safina? (Mwa. 8:6-12) (12) Noa alifanya nini alipotoka kwenye safina? (Mwa. 8:20-22) (13) Upinde wa mvua unawakilisha nini? (Mwa. 9:8-16) (14) Inamaanisha nini ‘kutembea pamoja na Mungu’? (Mwa. 6:9, 22; 7:5) (15) Tunapaswa kufanya nini ili tumwone Noa katika Paradiso? (Mt. 28:19, 20; 1 Pet. 2:21)

Simulizi la Biblia kuhusu Noa ambaye alikuwa mwaminifu na mtiifu, limekufundisha nini kuhusu jinsi ambavyo wewe pia unaweza ‘kutembea pamoja na Mungu’ na kuwa na uhakika katika nguvu za Yehova za kuwaokoa watu wake wa siku hizi?—Mwa. 7:1; Met. 10:16; Ebr. 11:7; 2 Pet. 2:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki