Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/06 uku. 6
  • Roho ya Kujitolea Huleta Baraka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Roho ya Kujitolea Huleta Baraka
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Misaada Yatolewa Kotekote Duniani
    Amkeni!—2001
  • Wafanyakazi wa Kujitolea Kazini
    Amkeni!—2001
  • “Acheni Sisi Tufanye Lililo Jema Kuelekea Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kazi ya Kujitolea Yenye Faida ya Kudumu
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 12/06 uku. 6

Roho ya Kujitolea Huleta Baraka

1 Goliathi alipoyadhihaki majeshi ya Israeli, askari yeyote angepigana naye. Lakini hakuna aliyejitolea isipokuwa mvulana mchungaji ambaye hakuwa amezoezwa kwa ajili ya vita. (1 Sam. 17:32) Wayahudi waliohamishwa waliporudi Yerusalemu lakini wakashindwa kujenga upya kuta zake, ni mnyweshaji wa mfalme wa Uajemi ambaye alijitolea kuacha cheo chake katika nyumba ya mfalme kwenda Yerusalemu akasimamie kazi. (Neh. 2:5) Yehova aliwabariki Daudi na Nehemia kwa sababu ya roho waliyoonyesha.—1 Sam. 17:45, 50; Neh. 6:15, 16.

2 Leo, hakuna roho ya kujitolea ulimwenguni. Katika hizi “siku za mwisho,” watu huishi maisha yenye shughuli nyingi, na wengi ‘hujipenda wenyewe.’ (2 Tim. 3:1, 2) Ni rahisi kwa mtu kujihusisha sana katika mapendezi ya kibinafsi hivi kwamba anapuuza nafasi za kujitolea wengine wanapohitaji msaada. Hata hivyo, tukiwa Wakristo, tunatamani kumwiga Yesu, ambaye alichukua hatua kuwasaidia wengine. (Yoh. 5:5-9; 13:12-15; 1 Pet. 2:21) Tunaweza kuonyeshaje roho ya kujitolea, na tutapata baraka gani?

3 kwa Ajili ya Ndugu Zetu: Tunaweza kuwapa wengine “zawadi ya kiroho” kwa kujitolea kutoa maelezo kunapokuwa na sehemu katika mikutano inayohitaji maelezo kutoka kwa wasikilizaji. (Rom. 1:11) Kutoa maelezo kunamletea Yehova heshima, kunasaidia kukaza ukweli ndani ya akili na mioyo yetu, na kunatusaidia tufurahie mikutano zaidi. (Zab. 26:12) Vilevile tunaweza kujitolea kutoa hotuba katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi yule aliyegawiwa anaposhindwa kuitoa. Hilo litatusaidia kuboresha uwezo wetu wa kufundisha.

4 Akina ndugu wanaweza kuonyesha roho ya kujitolea kwa kujitahidi kufikia madaraka zaidi kutanikoni. (Isa. 32:2; 1 Tim. 3:1) Sisi sote tunaweza kuchangia kufanikiwa kwa programu za makusanyiko ya wilaya na ya mzunguko kwa kujitolea kufanya kazi katika idara mbalimbali. Tunapojitolea kuhubiri na mwangalizi anayesafiri au kumwandalia mlo, tunaweza kuwa na “ubadilishanaji wa kitia-moyo.” (Rom. 1:12) Tunapowasaidia wavulana wasio na baba, wajane, wagonjwa, walio dhaifu, akina mama wenye watoto wadogo, na wengine kutanikoni, tunapata shangwe na kibali cha Yehova.—Met. 19:17; Mdo. 20:35.

5 Njia nyingine ambayo tunaweza kutoa wakati na nguvu zetu ni kusaidia kusafisha na kudumisha Jumba la Ufalme. Isitoshe, kwa kuwa watu wengi sana wanakubali kweli, kuna uhitaji unaoongezeka wa kujenga Majumba ya Ufalme. Hivyo, watu wa kujitolea kuyajenga wanahitajika pia. Wenzi fulani wa ndoa walijitolea kusaidia Halmashauri ya Ujenzi ya Mkoa hata ingawa hawakuwa na uzoefu wowote wa ujenzi. Baada ya muda, wenzi hao walizoezwa na sasa wao husaidia kujenga kuta. Mke alisema hivi: “Kufanya kazi na wengine kumetusaidia tuwe na marafiki wa karibu. Siku inapokwisha, tunakuwa tumechoka kimwili lakini tumeburudika kiroho.”

6 kwa Kuhubiri: Kazi muhimu zaidi ya kujitolea ambayo tunaweza kufanya leo ni ile ya kuhubiri kuhusu Ufalme. Watu wanaposaidiwa kuelewa na kutumia mashauri ya Biblia, wanapata kusudi maishani na nguvu za kukabiliana na mazoea yenye kudhuru. Wanajifunza tumaini la wakati ujao lenye kutia moyo. Kwa kutoa elimu ya Biblia, tunafanya kazi ya kujitolea ambayo huleta shangwe na manufaa ya kudumu. (Yoh. 17:3; 1 Tim. 4:16) Huenda hali zetu zikaturuhusu tufanye kazi hiyo kwa njia kubwa zaidi kwa kuwa mapainia-wasaidizi au mapainia wa kawaida, kwa kuhamia mahali palipo na uhitaji mkubwa, au kwa kujifunza lugha nyingine.

7 Mfalme Daudi alitabiri kwamba wakati ambapo Masihi ataanza kutawala, watu wa Mungu “watajitoa kwa hiari.” (Zab. 110:3) Yehova anapoharakisha mavuno ya mwisho ya kiroho, kuna kazi nyingi zaidi ambayo lazima tujitolee. (Isa. 60:22) Je, umesema: “Mimi hapa! Nitume mimi”? (Isa. 6:8) Kwa kweli, tunapoonyesha roho ya kujitolea, tunampendeza Yehova na kuvuna baraka tele.

[Maswali ya Funzo]

1. Daudi na Nehemia walionyeshaje roho ya kujitolea?

2. Kwa nini Wakristo wanapaswa kuonyesha roho ya kujitolea?

3. Roho ya kujitolea inahusikaje katika mikutano ya kutaniko?

4. Ni katika njia gani nyingine tunaweza kuonyesha roho ya kujitolea?

5. Ni mambo gani kuhusu Majumba ya Ufalme yanayohitaji wajitoleaji wa hiari?

6. Kwa nini kazi ya kuhubiri ndiyo kazi muhimu zaidi ya kujitolea tunayoweza kufanya?

7. Kwa nini kujitolea ni muhimu hasa leo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki