Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/07 uku. 1
  • Wote Wanaweza Kushiriki Kufanya Wanafunzi Wapya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wote Wanaweza Kushiriki Kufanya Wanafunzi Wapya
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Mkiwa Kutaniko, Wasaidieni Wanafunzi wa Biblia Wafikie Hatua ya Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kuwasaidia Wengine Washike Amri za Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • “Basi, Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 4/07 uku. 1

Wote Wanaweza Kushiriki Kufanya Wanafunzi Wapya

1 Mwanafunzi mpya hapatikani kwa sababu ya jitihada za mtu mmoja tu. Ili kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wakue kiroho, Yehova anaweza kutumia wote kati ya “wafanyakazi wenzi” wake. (1 Kor. 3:6-9) Sisi mmoja-mmoja tunaweza kuwasaidia wapya kwa kutoa maelezo katika mikutano ya Kikristo na vilevile kwa mwenendo wetu mzuri ambao huonyesha wazi kwamba roho ya Mungu inafanya kazi katika maisha yetu. (Yoh. 13:35; Gal. 5:22, 23; Efe. 4:22, 23) Ni nini kingine tunachoweza kufanya kuwasaidia wapya?

2 Kama Kutaniko: Sisi sote tunaweza kuonyesha tunapendezwa na wale wanaoanza kuhudhuria mikutano kwa kuchukua hatua ya kuwasalimu kwa uchangamfu na kuzungumza nao kabla na baada ya mikutano. Akikumbuka kuhusu mara ya kwanza alipohudhuria mikutano, mwanamume mmoja alisema: “Tofauti na watu wote ambao nimewahi kukutana nao katika kanisa nililolelewa, siku hiyo moja nilikutana na watu wenye upendo wa kweli ingawa sikuwa nimewafahamu hata kidogo. Ilikuwa wazi kwamba nilikuwa nimepata kweli.” Alibatizwa miezi saba baada ya kuhudhuria mkutano huo wa kwanza.

3 Toa pongezi ya kweli mwanafunzi wa Biblia anapofanya maendeleo ya kiroho. Je, amekuwa akivumilia upinzani? Je, anahudhuria mikutano kwa ukawaida? Je, anajipa ujasiri wa kutoa maelezo? Je, amejiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi au ameanza kushiriki katika huduma? Mpongeze kwa maendeleo ambayo amefanya. Hilo litamburudisha na kumtia moyo.—Met. 25:11.

4 Kama Kiongozi wa Funzo la Biblia: Wahubiri fulani wameweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia kufahamiana na washiriki mbalimbali wa kutaniko kwa kuwaomba wahubiri wengine waandamane nao kwenye funzo. Mkaribishe mwanafunzi ahudhurie mikutano ya kutaniko haraka iwezekanavyo. Anapoanza kuhudhuria mikutano, msaidie awafahamu wengine. Je, anajitahidi kushinda zoea fulani baya, kama vile kuvuta sigara? Je, kuna mtu fulani nyumbani kwao anayepinga kujifunza kwake? Anaweza kunufaika kwa kuzungumza na mhubiri ambaye amekabili na kushinda tatizo kama hilo.—1 Pet. 5:9.

5 Wapya wanahitaji msaada wa kiroho kutoka kwa wote kutanikoni. Kila mmoja anaweza kuwasaidia kufanya maendeleo kwa kuwaonyesha kwamba tunapendezwa nao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki