Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/07 uku. 1
  • Endelea “Kuzaa Matunda Mengi”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea “Kuzaa Matunda Mengi”
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Fulizeni Kuzaa Matunda Mengi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kuonea Shangwe Uhusiano wa Karibu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kuzaa Matunda Kunakomtukuza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Rafiki za Yesu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 6/07 uku. 1

Endelea “Kuzaa Matunda Mengi”

1 Akitumia maneno ya mfano, Yesu alijifananisha na mzabibu wa kweli, akamfananisha Baba yake na Mkulima, naye akawafananisha wafuasi wake waliotiwa mafuta kwa roho na matawi ya mzabibu yanayozaa matunda. Akifafanua kazi ya Mkulima huyo wa mfano, Yesu alikazia umuhimu wa kuendelea kushikamana kabisa na mzabibu. (Yoh. 15:1-4) Kupitia mfano huo, tunajifunza kwamba kila mtu aliye na uhusiano wa karibu na Yehova lazima awe kama tawi lenye kuzaa matunda la “mzabibu wa kweli,” Yesu Kristo. Lazima tuendelee kuzaa “matunda ya roho” na matunda ya Ufalme kwa wingi.—Gal. 5:22, 23; Mt. 24:14; 28:19, 20.

2 Matunda ya Roho: Maendeleo yetu ya kiroho yanaweza kupimwa hasa kwa kutegemea kadiri ambavyo tunaonyesha matunda ya roho. Je, wewe hujitahidi kusitawisha matunda ya roho ya Mungu kwa kujifunza na kutafakari Neno la Mungu kwa ukawaida? (Flp. 1:9-11) Usisite kusali ili upate roho takatifu inayoweza kukusaidia kusitawisha sifa zinazomtukuza Yehova na zitakazokusaidia kuendelea kufanya maendeleo ya kiroho.—Luka 11:13; Yoh. 13:35.

3 Kusitawisha matunda ya roho kutatusaidia pia kuwa wahudumu wenye bidii zaidi. Kwa mfano, upendo na imani hutuchochea kutenga wakati katika maisha yetu yenye shughuli nyingi ili tushiriki kwa ukawaida katika huduma. Sifa kama vile amani, ustahimilivu, fadhili, upole, na kujizuia, hutusaidia kutenda ifaavyo tunapopingwa. Shangwe hutuwezesha kupata uradhi katika huduma hata watu wasipopendezwa.

4 Matunda ya Ufalme: Tunataka pia kuzaa matunda ya Ufalme. Hiyo inahusisha kutoa “dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo ambayo hulifanyia jina [la Yehova] tangazo la hadharani.” (Ebr. 13:15) Tunafanya hivyo kwa kutangaza habari njema kwa bidii na usadikisho. Je, unajitahidi kuzaa matunda mengi zaidi ya Ufalme kwa kuboresha huduma yako?

5 Yesu alionyesha kwamba wafuasi wake waaminifu wangezaa kiasi tofauti-tofauti cha matunda. (Mt. 13:23) Hivyo, hatupaswi kujilinganisha na wengine bali tunapaswa kumpa Yehova kilicho bora. (Gal. 6:4) Kuchunguza hali zetu kwa unyoofu kwa kutumia Neno la Mungu kutatusaidia kuendelea kumtukuza Yehova kwa “kuzaa matunda mengi.”—Yoh. 15:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki