Tutatoa Toleo la Pekee la Amkeni! Mwezi wa Novemba!
1 Watu wengi wana maswali ya unyoofu kuhusu thamani ya Biblia. Ikiwa wanadamu ndio walioiandika, inawezaje kuitwa Neno la Mungu? Kwa nini niitegemee ili iongoze hatua zangu? Nikitumia wakati na jitihada kusoma na kujifunza Biblia, nitapata thawabu gani? Nitumie tafsiri gani ya Biblia? Hayo ni baadhi ya maswali ambayo yanajibiwa katika toleo la pekee la Amkeni! la Novemba lenye kichwa “Je, Unaweza Kuitegemea Biblia?”
2 Tungependa kusambaza sana toleo hilo la pekee la Amkeni! katika eneo letu. Ikiwezekana, shiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba kila Jumamosi pamoja na kutaniko katika mwezi wa Novemba. Waonyeshe toleo hilo la pekee la Amkeni! watu wako wa ukoo, majirani, wafanyakazi wenzako, walimu, wanafunzi wenzako, na wale ambao umepanga kuwarudia. Beba nakala kadhaa unapokwenda sokoni na unaposafiri. Kuna magazeti ya ziada ili kutaniko liweze kuwa na nakala za kutosha.
3 Anzisha Funzo la Biblia: Ukiacha gazeti, unaweza kuweka msingi wa funzo la Biblia kabla ya kumaliza mazungumzo. Kwa mfano, unaweza kusema, “Wakati ujao, ningependa kukuonyesha jibu la Biblia kwa swali hili, ‘Ni nini kusudi la Mungu kwa dunia?’” Kisha rudi ukiwa na kitabu Biblia Inafundisha na umwonyeshe mwenye nyumba ukurasa wa 4-5, au uzungumzie mafungu ya 1-3 ya sura ya 3. Au unaweza kusema, “Wakati ujao, ningependa kuzungumzia unabii wa Biblia ambao unatimizwa sasa hivi.” Unaporudi, mwonyeshe mwenye nyumba sura ya 9 ya kitabu hicho na mzungumzie mafungu ya 1-3. Au unaweza tu kumweleza mwenye nyumba: “Watu wengi huona ni vigumu kuelewa mambo wanayosoma katika Biblia. Wakati ujao, ningependa kukuonyesha jinsi unavyoweza kuelewa Biblia yako vizuri zaidi.” Kwenye ziara ya kurudia, mwonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, na umwelekeze jinsi funzo linavyoongozwa.
4 Ni Biblia pekee ambayo ina “maandishi matakatifu,” yanayoweza kutufanya tuwe ‘wenye hekima kwa ajili ya wokovu.’ (2 Tim. 3:15) Hivyo, sisi sote tungependa kushiriki kwa bidii katika kusambaza toleo hilo la pekee la Amkeni! ili kuwasaidia watu waweze kuitegemea Biblia!