Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Kuongezeka kwa misiba ya asili leo kumefanya watu fulani wajiulize ikiwa Mungu anatuadhibu. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu. Kisha soma 1 Yohana 4:8.] Makala hii inaeleza kwa nini si Mungu anayesababisha mateso yanayoletwa na misiba ya asili.” Zungumzia makala iliyo kwenye ukurasa wa 30.
Amkeni! Mei
Soma Mathayo 6:10. Kisha uliza: “Je, umewahi kujiuliza mapenzi ya Mungu ni nini kuelekea dunia? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, tangu mwanzoni Mungu alikuwa na kusudi kuelekea dunia na kusudi hilo halijabadilika. Makala hii inazungumzia jambo hilo.” Zungumzia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Moja ya masimulizi ya Biblia yanayojulikana sana ni lile la Noa na Gharika. Je, unafikiri kweli kulikuwa na Gharika? [Mruhusu ajibu.] Inapendeza kujua kwamba Yesu alitaja kwamba kulikuwa na Gharika. [Soma Luka 17:26, 27.] Gazeti hili linatoa sababu za kuamini simulizi kuhusu Gharika na linaeleza mambo muhimu tunayoweza kujifunza kutokana na Gharika hiyo.”
Amkeni! Juni
“Kulea mtoto si kazi rahisi, hasa anapobalehe na kupatwa na mabadiliko makubwa. Unafikiri ni wapi ambapo wazazi wanaweza kupata mashauri yenye kutegemeka? [Mruhusu ajibu.] Kisha soma Isaya 48:17, 18.] Gazeti hili linatoa mapendekezo fulani ya hivi karibuni ili kuwasaidia wazazi kutenda kwa hekima na kuwaelewa watoto wao.”