Sanduku la Swali
◼ Je, inafaa makutaniko au mtu mmoja-mmoja atumie nembo za mashirika ya kisheria zinazotumiwa na Mashahidi wa Yehova?
Nembo ni jina, ishara, au alama ya utambulisho. Nembo ya Watch Tower inawakilisha shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania na mashirika mengine yanayotumiwa na tengenezo. Katika barua rasmi za tengenezo kuna barua zenye nembo ya Biblia iliyofunguliwa. Barua rasmi kutoka mashirika mengine yanayotumiwa na Mashahidi wa Yehova zina nembo tofauti-tofauti.
Makutaniko au mtu mmoja-mmoja hapaswi kutumia nembo au majina ya mashirika ya kisheria ya tengenezo, au kutumia alama zinazofanana na nembo hizo kwenye Majumba yao ya Ufalme, vibao, barua, vitu vya mtu binafsi, na kadhalika. Nembo za tengenezo zinapotumiwa kwa njia kama hizo, wenye mamlaka, wahubiri, na watu wengine wanaweza kuchanganyikiwa kuhusu uhusiano wa kisheria kati ya kutaniko na mashirika ya kisheria ya tengenezo. Vivyo hivyo, barua zinaweza kuonekana kimakosa kuwa zimeidhinishwa au kutumwa kutoka ofisi ya tawi au makao makuu ya ulimwengu.
Wakati ujao, nembo ya Watch Tower, au alama nyingine inayofanana nayo, haipaswi kuwekwa kwenye Jumba la Ufalme, hata kama jumba hilo linamilikiwa na shirika la Watch Tower. Makutaniko yaliyo na Majumba ya Ufalme ambayo yana nembo hayahitaji kuondoa alama hizo mara moja, kwa kuwa huenda kufanya hivyo kukahusisha mabadiliko makubwa yanayochukua wakati mwingi, na ambayo yanahusisha kazi nyingi na gharama kubwa. Hata hivyo, ndugu wanapaswa kufikiria kubadili alama hizo ikiwa mabadiliko yanayofanywa ni madogo na kazi haitakuwa nyingi. Lakini ikiwa mabadiliko ni makubwa, wanaweza kungoja hadi pale Jumba la Ufalme au sehemu nyingine zenye nembo hizo zitakapofanyiwa ukarabati.