Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/09 uku. 1
  • Je, Uko Tayari Kuhubiri Isivyo Rasmi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Uko Tayari Kuhubiri Isivyo Rasmi?
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Unaweza Kuhubiri Isivyo Rasmi!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Ongea Juu ya Utukufu wa Umaliki wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Iweni na Bidii Katika “Kutoa Ushahidi Kamili”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 10/09 uku. 1

Je, Uko Tayari Kuhubiri Isivyo Rasmi?

1. Ni mfano gani unaoonyesha kwamba kuhubiri isivyo rasmi kunaweza kuwa na matokeo mazuri?

1 Kuhubiri isivyo rasmi kunaweza kuwa na matokeo mazuri sana. Katika Biblia kuna mifano mingi ya watu waliohubiri isivyo rasmi na kupata matokeo mazuri. (Yoh. 4:7-15) Tunaweza kufanya nini ili kujitayarisha kuhubiri isivyo rasmi?

2. Mavazi na mapambo yetu yanawezaje kutusaidia katika kutoa ushahidi?

2 Mavazi na Mapambo: Tukiwa waangalifu kuhusiana na jinsi tunavyovalia na kujipamba, tutajihisi huru kuwaeleza wengine kuhusu imani yetu. (1 Tim. 2:9, 10) Ikiwa tunahisi kwamba hatujavalia vizuri kuweza kumwakilisha Yehova, huenda tukasita kutoa ushahidi. Lakini, tunapokuwa safi na nadhifu, huenda watu wakataka kujua kwa nini tumevalia tofauti na wengine. Kwa mfano, mume na mke waliovalia vizuri waliketi karibu na mwanamume Mwislamu walipokuwa safarini. Alipoona jinsi walivyokuwa wamevalia, mwanamume huyo aliwauliza ikiwa wao ni Wakristo. Swali hilo lilifanya wazungumzie Biblia kwa muda wa saa tatu.

3. Kwa kumwiga Yesu, umewezaje kuanzisha mazungumzo?

3 Kuanzisha Mazungumzo: Yesu alipokutana na mwanamke Msamaria kwenye kisima cha Yakobo, alianzisha mazungumzo kwa kumwomba tu maji ya kunywa. Vivyo hivyo, tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa kutaja jambo fulani kifupi au kwa kuuliza swali rahisi. Huenda nyakati nyingine tukasitasita, lakini kwa kutegemea msaada wa Yehova, tunaweza ‘kujipa ujasiri’ wa kuanzisha mazungumzo.—1 The. 2:2.

4. Tunaweza kujitayarishaje kuhubiri isivyo rasmi?

4 Kutafuta Nafasi: Wahubiri wengi wamepata njia mbalimbali za kuhubiri isivyo rasmi. Changanua hali zako, na uwafikirie watu ambao yaelekea unakutana nao kila siku. Beba vitabu vinavyofaa na Biblia ndogo. Uwe macho, na upendezwe na watu walio karibu nawe. Unapofikiria kimbele nafasi unazoweza kutumia kuwahubiria watu, yaelekea utakuwa tayari kutoa ushahidi kwa njia nzuri.—Flp. 1:12-14; 1 Pet. 3:15.

5. Kwa nini tunapaswa kuwa na mipango mizuri kuhusiana na mahubiri yasiyo rasmi?

5 Tuna sababu mbili nzuri za kutumia nafasi tunazopata kuhubiri isivyo rasmi—upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani. (Mt. 22:37-39) Kwa kuzingatia uhitaji wa haraka wa kuhubiri, tunapaswa kuwa na mipango mizuri kuhusiana na mahubiri yasiyo rasmi. Tunapaswa kuwa tayari kutumia nafasi yoyote inayofaa kuwahubiria wengine habari njema za Ufalme maadamu kuna wakati.—Rom. 10:13, 14; 2 Tim. 4:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki