Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/10 uku. 4
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Utegemezo kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kuwathamini Mapainia Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Kikumbusha kwa Mwandishi na Mwangalizi wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Baraka za Huduma ya Upainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 11/10 uku. 4

Sanduku la Swali

◼ Tunaweza kuwasaidia mapainia katika njia zipi?

Katika mwaka wa utumishi wa 2009, kulikuwa na ndugu na dada karibu 800,000 waliotumika wakiwa mapainia wa kawaida na wa pekee ulimwenguni pote. Watumishi hawa wa wakati wote, wanadhabihu matunda yao ya kwanza kwa kutumia wakati, nguvu, na mali zao ili kueneza habari njema za Ufalme. (Met. 3:9) Yehova anafurahishwa kama nini na jitihada zao! Ni katika njia gani tunaweza kuwa na maoni kama ya Yehova na kusaidia mapainia wetu kupata shangwe na kuvumilia katika utumishi wao?

Bila shaka, maneno yetu mazuri yanaweza kuwatia moyo kuendelea kutumika wakiwa mapainia. (Met. 25:11) Je, tunaweza kubadili ratiba yetu ya kila juma ili tuhubiri pamoja nao? Tunapohubiri pamoja nao, tunaweza kupendekeza kutumia gari letu badala ya lao au kuwalipia nauli. Na ikiwa tutasafiri nao kwa gari lao, labda tunaweza kuchangia kidogo kwa ajili ya matumizi yao. (1 Kor. 13:5; Flp. 2:4) Tunaweza pia kuwaonyesha upendo kwa kuwaonyesha ukarimu na kuwakaribisha nyumbani mara kwa mara kwa ajili ya mlo.—1 Pet. 4:8, 9.

Maandiko yanatoa uhakikisho kwamba Yehova ataandaa mahitaji ya kimwili kwa ajili ya wale wanaotafuta Ufalme wake kwanza. (Zab. 37:25; Mt. 6:33) Njia moja ambayo Yehova hufanya hivyo ni kupitia undugu wetu wa Kikristo wenye upendo. (1 Yoh. 3:16-18) Ni kweli kwamba mapainia hawatazamii majukumu yao ya kifedha yashughulikiwe na wengine. Na hata huenda wasiwe tayari kuwaambia wengine wanapokuwa na uhitaji fulani. Hata hivyo, tunaweza kuwasaidia mapainia waaminifu na ‘kujazia upungufu wao’ kwa kuwa macho na wenye utambuzi.—2 Kor. 8:14, 15.

Fibi, mweneza-injili wa karne ya kwanza kutoka Kutaniko la Kenkrea alipotembelea mji wa Roma, Paulo aliwatia moyo hivi ndugu wa Roma: “Mkamkaribishe katika Bwana kwa njia inayowastahili watakatifu, na . . . mkamsaidie katika jambo lolote ambalo huenda akawahitaji ninyi.” (Rom. 16:1, 2) Tuna fursa ya kuonyesha utegemezo kama huo wenye upendo kwa kina ndugu na dada wa kutaniko letu, wanaotangaza habari njema bila kuacha wakiwa mapainia wa kawaida na wa pekee.—Mdo. 5:42.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki