Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/12 uku. 2
  • Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • “Nimeyatia Maneno Yangu Katika Kinywa Chako”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Siwezi Kunyamaza Kimya”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Nitaishibisha Nafsi Iliyochoka”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 5/12 uku. 2

Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia

1. Ni kitabu gani kilichotolewa kwenye kusanyiko la wilaya mwaka wa 2010, na tutakitumiaje?

1 Tulisisimka kama nini wakati kitabu Mungu Asema Nasi kupitia Yeremia kilipotolewa kwenye Kusanyiko la Wilaya la 2010 lenye kichwa “Kaa Karibu na Yehova!” Kitabu hicho kinakazia fikira mambo yanayopatikana katika vitabu vya Yeremia na Maombolezo, ambayo yanaweza kutusaidia katika maisha yetu ya kila siku. (Rom. 15:4) Kimekusudiwa kwa ajili ya Funzo la Biblia la Kutaniko, na hivyo kitazungumziwa katika juma linaloanza Novemba 5, 2012.

2. Kwa nini tunaweza kufaidika kwa kuchunguza vitabu vya Biblia vya Yeremia na Maombolezo?

2 Ni Chenye Faida Leo: Yeremia, ambaye ndiye mwandikaji wa kitabu cha Biblia kilichoongozwa na roho ya Mungu chenye jina hilo, alikuwa akitoa unabii katika kipindi chenye misukosuko huko Yuda. Mwanzoni, alihisi kwamba hastahili kupewa mgawo huo. (Yer. 1:6) Aliteswa pia na marafiki na huenda hata watu wake wa ukoo kutoka Anathothi, mji wake wa nyumbani. (Yer. 11:21, 22) Inaeleweka kwamba pindi nyingine Yeremia alivunjika moyo. (Yer. 20:14) Tunapotimiza kazi yetu ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ mara kwa mara tunakabili hali ngumu na hisia sawa na zile za Yeremia. (Mt. 28:19) Kuchunguza mambo aliyoandika kutatusaidia kuitimiza huduma yetu tukiwa na ujasiri na bidii.

3. Tutatumiaje mambo fulani yanayopatikana katika kitabu Yeremia?

3 Yaliyomo: Maandiko yanayokazia mambo makuu ambayo yanapaswa kusomwa wakati wa mazungumzo yameandikwa katika italiki. Mwishoni mwa funzo la kila juma kuna swali moja au mawili makuu yaliyoandikwa kwa herufi nzito ambayo yanakazia mambo makuu katika funzo hilo. Wasikilizaji wanapaswa kuulizwa maswali hayo kwa njia ya pitio. Kitabu chote kina picha nzuri ambazo pasipo shaka wasikilizaji wangependa kuzielezea.

4. Tunaweza kufaidikaje kikamili tunapochunguza kitabu Yeremia?

4 Ili kufaidika kwa ukamili, tayarisha mapema sehemu itakayozungumziwa. Tafuta mambo unayoweza kutumia katika maisha na huduma yako. Shiriki kikamili kutoa maelezo. Yehova alimbariki Yeremia, na hivyo akatimiza mgawo wake kwa shangwe na uradhi. (Yer. 15:16) Acheni kuchunguza kitabu hiki kipya kutusaidie kutimiza huduma yetu kwa njia hiyohiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki