Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/12 uku. 1
  • Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Anawapenda Wale ‘Wanaozaa Matunda kwa Uvumilivu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • ‘Fulizeni Kuzaa Matunda Mengi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • ‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Usife Moyo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 11/12 uku. 1

Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu

1. Ni jambo gani linaloweza kutufanya tupunguze bidii yetu katika huduma?

1 Mwanadamu aliumbwa ili aone “mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.” (Mhu. 2:24) Hata hivyo, tunapokosa kuona mema katika huduma yetu, tunaweza kupoteza shangwe na kupunguza bidii yetu kwa sababu ya kuvunjika moyo. Ni nini kinachoweza kutusaidia kudumisha mtazamo unaofaa?

2. Kwa nini tunapaswa kuwa na matarajio yenye usawaziko kuhusiana na jinsi watu wanavyoitikia huduma yetu?

2 Uwe na Matarajio Yenye Usawaziko: Kumbuka kwamba ingawa ni watu wachache tu walioitikia vizuri mafundisho ya Yesu, hakuna shaka kwamba alipata matokeo mazuri katika huduma yake. (Yoh. 17:4) Katika mfano wake wa mpandaji, Yesu alitabiri kwamba mioyo ya watu wengi haingeweza kuitikia ujumbe wa Ufalme ulio kama mbegu. (Mt. 13:3-8, 18-22) Licha ya hali hiyo, jitihada zetu nyingi bado zinatimiza mambo mengi.

3. Tunaweza ‘kuzaa matunda’ jinsi gani hata watu wasipoitikia vizuri kazi yetu ya kuhubiri?

3 Jinsi Tunavyozaa Matunda Mengi: Kulingana na mfano wa Yesu, wale wanaokubali ujumbe wa Ufalme ‘wangezaa matunda.’ (Mt. 13:23) Baada ya bua la ngano kuota na kukomaa, linazaa matunda, yaani mbegu mpya, wala halizai mabua madogo ya ngano. Kwa hiyo, matunda ambayo Mkristo mwenye matokeo mazuri anazaa si lazima yawe wanafunzi wapya, bali ni mbegu zaidi za Ufalme, yaani, kuzungumza juu ya Ufalme huo. Kufanya hivyo hutokeza “mema” ambayo yanatufanya turidhike, iwe watu wanaitikia vizuri au la. Tunachangia kutakaswa kwa jina la Yehova. (Isa. 43:10-12; Mt. 6:9) Tunafurahia pendeleo la kuwa wafanyakazi wenzi wa Mungu. (1 Kor. 3:9) Na “tunda [hilo] la midomo” humpendeza Yehova.—Ebr. 13:15, 16.

4. Ni matokeo gani tusiyoweza kuyaona ambayo huenda tukapata katika huduma yetu?

4 Kwa kuongezea, huenda jitihada zetu zikawa na matokeo ambayo hatuyaoni. Inawezekana kwamba baadhi ya watu ambao walimsikia Yesu akihubiri walikuja kuwa wanafunzi wake baada ya Yesu kukamilisha huduma yake duniani. Vivyo hivyo, mbegu ya Ufalme ambayo tunapanda huenda isitie mizizi na kukua moyoni mwa mtu hadi wakati mwingine, na mtu huyo anaweza kuwa Shahidi wa Yehova bila sisi kujua. Kwa kweli, huduma yetu hutimiza mambo mengi mema. Hivyo basi, na ‘tuendelee kuzaa matunda mengi’ na kujithibitisha wenyewe kuwa wanafunzi wa Yesu.—Yoh. 15:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki