Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/13 uku. 1
  • “Toa Ushahidi Kamili”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Toa Ushahidi Kamili”
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Aliazimia Kutoa Ushahidi Kamili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Iweni na Bidii Katika “Kutoa Ushahidi Kamili”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Twazoezwa Kutoa Ushahidi Kamili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Hubiri na Kutoa Ushahidi Kamili
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 1/13 uku. 1

“Toa Ushahidi Kamili”

1. Mtume Paulo aliweka mfano gani mzuri katika huduma?

1 “Timiza kikamilifu utumishi wako.” (2 Tim. 4:5, Biblia Habari Njema) Kwa hakika, mtume Paulo alikuwa na uhuru wa kusema alipokuwa akimpa Timotheo himizo hilo. Isitoshe, Paulo alimaliza safari tatu za umishonari kati ya mwaka wa 47 na 56 W.K. Kitabu cha Matendo hutaja tena na tena kwamba Paulo alitoa “ushahidi kamili.” (Mdo. 23:11; 28:23) Tunawezaje kufanya hivyo leo?

2. Tunawezaje kutoa ushahidi kamili tunapohubiri nyumba kwa nyumba?

2 Nyumba kwa Nyumba: Katika jitihada za kuwapata wenye nyumba ambao hawajawahi kusikia habari njema, huenda tukahitaji kuwatembelea watu wakati tofauti. Huenda kichwa cha familia akapatikana nyumbani saa za jioni au mwisho-juma. Tunapaswa kujitahidi kumhubiria mtu fulani katika kila nyumba, na kurudi tena na tena kwenye nyumba ambazo tumekosa watu. Vipi ikiwa hujafanikiwa kumpata mtu yeyote nyumbani licha ya jitihada zako? Labda unaweza kupata matokeo mazuri kwa kuandika barua au kupiga simu.

3. Wewe una nafasi gani za kutoa ushahidi hadharani na isivyo rasmi?

3 Hadharani na Isivyo Rasmi: Leo, watumishi wa Yehova huwajulisha “hekima ya kweli” watu wote watakaosikiliza. Nyakati nyingine, wao hufanya hivyo “barabarani” au “katika viwanja vya watu wote.” (Met. 1:20, 21) Je, tuko macho kutoa ushahidi tunapokuwa katika shughuli zetu za kila siku? Je, inaweza kusemwa kuwa sisi ni wenye “kushughulika sana na lile neno”? (Mdo. 18:5) Ikiwa ndivyo ilivyo, basi tunatimiza wajibu wetu wa “kutoa ushahidi kamili.”​—Mdo. 10:42; 17:17; 20:20, 21, 24.

4. Sala na kutafakari hutusaidiaje kutoa ushahidi kamili?

4 Hata hivyo, nyakati nyingine kwa sababu ya udhaifu wetu au hali ya kuhisi haya ambayo tumerithi, huenda tukasita kutoa ushahidi. Bila shaka, Yehova anaelewa udhaifu wetu. (Zab. 103:14) Isitoshe, nafasi kama hizo zinapojitokeza, tunaweza kusali kwake ili tupate ujasiri wa kuzungumza. (Mdo. 4:29, 31) Pia, tunapofanya funzo la kibinafsi na kutafakari Neno la Mungu, tunaweza kukazia fikira kuongeza uthamini wetu kwa thamani bora zaidi ya habari njema. (Flp. 3:8) Hilo litatuchochea tutangaze habari njema kwa bidii!

5. Tunawezaje kushiriki katika kutimiza unabii wa Yoeli?

5 Unabii wa Yoeli ulitabiri kwamba kabla ya kuja kwa siku kuu yenye kutisha ya Yehova, watu wa Mungu ‘wangesonga mbele’ na hawangeruhusu kitu chochote kiwazuie kuhubiri. (Yoe. 2:2, 7-9) Na tufanye yote tuwezayo katika kazi hiyo ya kutoa ushahidi ambayo haitarudiwa kamwe!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki