Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Mei
“Sote tunafanana kwa njia moja yaani tunafanya makosa. Je, umewahi kufikiria ikiwa Mungu anaweza kusamehe hata makosa makubwa?” [Mruhusu ajibu.] Mwonyeshe makala iliyo katika ukurasa wa 15 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Tungependa kujua maoni yako kuhusu andiko hili. [Soma 1 Yohana 4:8.] Wengi wanakubaliana na maneno haya lakini wengine hufikiri kwamba lazima Mungu awe mkatili kwa kusababisha, au angalau kuruhusu misiba ya asili. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza vizuri kwa nini hatupaswi kumwelewa Mungu vibaya kuwa ni mkatili.”
Amkeni! Mei
“Tunawatembelea jirani zetu ili kuzungumzia tatizo la uhalifu linalowahangaisha watu wengi. Wengine hufikiri kwamba njia bora ya kudhibiti uhalifu ni kuongeza idadi ya polisi. Unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Je, ulijua kwamba Biblia inaahidi uhalifu utakomeshwa? [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili linazungumzia uhakika huo na linatupa baadhi ya hatua zinazofaa tunazoweza kuchukua ili kujilinda na uhalifu.”