Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Septemba
“Hujambo. Tumewatembelea kwa muda mfupi ili kuwaonyesha habari inayotegemeka inayoweza kuwasaidia watu waliofunga ndoa wafanikiwe. Kwa maoni yako, unafikiri ni nini kinachowafanya watu wakose furaha katika ndoa?” [Mruhusu ajibu.] Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti, na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
“Tunawatembelea kwa sababu watu wengi wanajiuliza kwa nini Mungu ameruhusu watu wateseke sana. Je, umewahi kufikiria jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Ni jambo linalotia moyo kuona kwamba Biblia inaahidi kuwa wakati ujao hakutakuwa na maombolezo wala maumivu. [Soma Ufunuo 21:4.] Gazeti hili linazungumzia sababu tano kwa nini watu wanateseka sana. Pia, linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi Mungu atakavyoondoa mateso.”
Amkeni! Septemba
“Tumewatembelea ili kuzungumza nanyi kuhusu sikukuu maarufu inayokaribia ya Halloween. Baadhi ya watu hawasherehekei sikukuu hiyo kwa sababu ya onyo hili la Biblia [Soma Mambo ya Walawi 19:31.] Wengine hawaamini ushirikina na hivyo hawaoni ubaya wowote wa kusherehekea sikukuu ya Halloween. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia chanzo kisichofaa cha sikukuu ya Halloween.”