Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/13 kur. 4-6
  • Mambo Yaliyoonwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo Yaliyoonwa
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Kusitawisha Kupendezwa na Ujumbe wa Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 12/13 kur. 4-6

Mambo Yaliyoonwa

◼ Australia: Mwanamume msomi anayeitwa John, alikuwa akienda kanisani alipokuwa mtoto, lakini baadaye akaacha “kumwamini Mungu kabisa.” Painia mmoja alimwachia broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? na katika ziara ya kurudia akamwachia broshua Chanzo cha Uhai. Painia huyo aliendelea kukuza upendezi wa mwanamume huyo kwa kumpelekea magazeti ya karibuni na kuzungumzia makala zote zinazohusu uumbaji au unabii wa Biblia. Alipoona kwamba John alikuwa tayari, alimwachia kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Baada ya kukisoma, John alianza “kujiona kwa kadiri fulani kuwa mtu anayeamini kwamba mambo ya Mungu hayajulikani.” Halafu painia huyo akamwonyesha kitabu Biblia Inafundisha, fungu la 8 ukurasa wa 20 na fungu la 13-16 ukurasa wa 23-24. Maandiko yaliyonukuliwa kwenye habari hiyo yalimvutia sana hivi kwamba alisema hivi: “Huenda ninahitaji tena kuichunguza Biblia.”

◼ Mexico: Mwanamume mmoja alimwambia mhubiri kuwa haamini kwamba Biblia imeandikwa kwa mwongozo wa Mungu. Mhubiri huyo alimsadikisha kwamba Biblia imeongozwa na roho ya Mungu. Baada ya kuzungumza naye mara kadhaa, mtu huyo akaanza kuguswa na mambo aliyokuwa anajifunza kutoka kwa Biblia, hasa mambo yaliyohusu viwango vya Mungu. Alimwambia mhubiri huyo hivi: “Mwanzoni tulipokuwa tukisoma Biblia pamoja, sikuona mashauri yake yakiwa tofauti na vitabu vingine vyovyote, hivyo, nilihisi kwamba hayanihusu. Hata hivyo, sasa tunaposoma Biblia, hasa mashauri kuhusu maadili, moyo wangu huchochewa sana.”

◼ Marekani: Walipokuwa wakishiriki katika Mpango wa Pekee wa Kuhubiri Hadharani Katika Miji Mikubwa, wenzi fulani wa ndoa walikutana na mwanamke kutoka Taiwan aliyemwamini Mungu lakini alifikiri kwamba Biblia ni kitabu cha watu wa Ulaya. Alisogelea meza ya machapisho kwa sababu alihisi kwamba amepoteza mwelekeo maishani ingawa alikuwa mwenye ufanisi. Alitumaini kwamba Biblia ingemsaidia apate kusudi maishani. Wenzi hao walianza kujifunza naye kitabu Biblia Inafundisha pamoja na broshua Lasting Peace and Happiness—How to Find Them. Badala ya kujifunza naye sura ya 2 ya kitabu hicho, walizungumzia sehemu ya broshua yenye kichwa “A Guidebook for the Blessing of All Mankind.” Baada ya kuzungumzia mafungu sita ya kwanza katika sehemu hiyo, mwanamke huyo alisema kwamba alivutiwa na jinsi Biblia ilivyo kitabu cha pekee tofauti na vitabu vingine vya kidini. Baada ya kuzungumzia unabii wa Biblia ambao tayari umetimia, alisema, “Hakuna kitabu kingine chochote kinachoweza kuwa sahihi kama Biblia!”

◼ Japani: Ingawa mwenye nyumba alimwambia mhubiri fulani kwamba hakumwamini Mungu, mhubiri huyo aliendelea kumtembelea na kuzungumzia naye kwa kifupi makala za Amkeni! zenye kichwa “Je, Ni Kazi ya Ubuni?” Hatua kwa hatua mwanamume huyo alianza kubadili maoni yake na kuanza kukubali kwamba huenda kuna Muumba. Sasa anaamini kwamba kuna Mungu, na anajifunza broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!

◼ Kanada: Mwanamke fulani alipokuwa akitoka nyumbani kuelekea kwenye gari lake, alikubali kupokea gazeti la karibuni zaidi kutoka kwa dada mmoja. Baadaye dada huyo alipomrudia, mwanamke huyo alimwambia waziwazi kuwa hapendezwi na hamwamini Mungu. Dada huyo aliazimia kutokata tamaa na akaamua kumpelekea broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha. Dada huyo alipompata mwanamke huyo nyumbani, alimwambia kwamba ingawa alijua kuwa mwanamke huyo hamwamini Mungu, bado alikuwa akimfikiria kwa sababu alijua kwamba mwanamke huyo ni mzazi mmoja. Hivyo alimwonyesha fungu la 6 kwenye ukurasa wa 4 wa broshua hiyo, linalozungumzia jinsi ya kupata mashauri mazuri. Halafu akamtia moyo asome mapendekezo yaliyo kwenye somo la pili yanayohusu kulea watoto. Mwanamke huyo alifurahi sana kupokea broshua hiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki