Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/14 uku. 1
  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Mika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Mika
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 33—Mika
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Tutatembea Katika Jina la Yehova Milele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Watumishi wa Yehova Wana Tumaini la Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Yehova Anataka Nini Kwetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 1/14 uku. 1

Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Mika

1. Mika alijiuliza swali gani, lakini kwa nini kazi yake ya kuhubiri haikuwa ya bure?

1 ‘Mwisho wa mfumo huu mbovu wa mambo utakuja lini?’ Huenda nabii Mika alifikiria swali kama hilo alipokuwa akitangaza ujumbe wa hukumu ya Yehova dhidi ya ufalme wa Israeli na Yuda. Hata hivyo, imani yake ilithawabishwa. Wakati wa maisha ya Mika, mwaka wa 740 K.W.K., maneno ya Yehova kuhusu Samaria yalitimia. (Mika 1:6, 7) Baadaye, Yerusalemu liliharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. (Mika 3:12) Tunaweza kumwiga Mika katika njia gani tunaposubiri kutimizwa kwa hukumu za Yehova katika siku zetu?

2. Tunaonyeshaje subira tunapoitazamia siku ya Yehova? Na kwa nini?

2 Uwe na Subira: Mika aliandika hivi: “Mimi, nitaendelea kumtazamia Yehova. Nitaonyesha mtazamo wa kumngojea Mungu wa wokovu wangu.” (Mika 7:7) Bila shaka, Mika hakukaa tu kitako akisubiri mwisho uje. Aliendelea kutangaza kwa bidii unabii wa Yehova. Tunaposubiri siku ya Yehova, tunapaswa pia kujihusisha katika “matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu.” (2 Pet. 3:11, 12) Subira ya Yehova inawapa watu mmoja-mmoja nafasi ya kutubu. (2 Pet. 3:9) Kwa hiyo, tunatii ushauri wa Biblia tunapowaiga manabii kwa kuwa na sifa ya subira.—Yak. 5:10.

3. Kwa nini tunapaswa kumwomba Yehova atupatie roho yake takatifu?

3 Tegemea Nguvu za Yehova: Ingawa, mgawo wa Mika ulikuwa na changamoto nyingi, alimtegemea Yehova ampe nguvu za kuutimiza. (Mika 3:8) Yehova anajua kwamba tunahitaji nguvu zake na ndiyo sababu katika Neno Lake tunatiwa moyo tumtegemee. Kwa ukarimu Yehova huwapa nguvu waliochoka ili watimize majukumu yao ya kitheokrasi. (Zab. 84:5, 7; Isa. 40:28-31) Je, wewe mwenyewe umejionea jambo hilo katika utumishi wako mtakatifu? Je, una kawaida ya kumwomba Yehova ili akusaidie na roho yake takatifu yenye nguvu?—Luka 11:13.

4. Tunajifunza nini kutokana na maisha ya Mika?

4 Mika alitanguliza kufanya mapenzi ya Mungu maishani mwake. Aliazimia kubaki mwaminifu licha ya kuzungukwa na upotovu mwingi wa maadili. Vivyo hivyo, uaminifu wetu unajaribiwa kila siku. Hivyo basi, na tuimarishe azimio letu la ‘kutembea katika jina la Yehova Mungu wetu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.’—Mika 4:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki