Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/14 kur. 5-6
  • Jinsi ya Kuwasaidia Wenye Tatizo la Kusoma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuwasaidia Wenye Tatizo la Kusoma
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Wafundishe Watu Wasioweza Kusoma Vizuri
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Wasaidie Wengine Watii Mambo Ambayo Biblia Inafundisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Jitahidi Uwe Msomaji Mzuri
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 6/14 kur. 5-6

Jinsi ya Kuwasaidia Wenye Tatizo la Kusoma

1. Tunapata changamoto gani tunapowafundisha Biblia watu wenye tatizo la kusoma?

1 Huenda wenye nyumba ambao wana matatizo ya kusoma wakapendezwa na mambo ya kiroho, lakini wakaogopa kujifunza Biblia na vitabu vingine. Huenda mwanzoni, tusipate matokeo mazuri ikiwa tutawaachia kitabu Biblia Inafundisha. Tunawezaje kuwasaidia watu hao wajifunze Biblia? Tuliwauliza wahubiri wenye uzoefu kutoka katika nchi zaidi ya 20 jinsi wao hushughulikia hali hiyo. Yafuatayo ni mapendekezo waliyotoa.

2. Ni machapisho gani tunayoweza kutumia ili tupate matokeo tunapowasaidia watu wenye tatizo la kusoma?

2 Ikiwa mwanafunzi ana tatizo la kusoma au hawezi kusoma, unaweza kuanza kujifunza naye broshua, Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele. Painia mmoja kutoka Marekani humwonyesha mwenye nyumba broshua zote mbili na kumuuliza ni ipi itamfaa zaidi. Ofisi ya tawi ya Kenya inaripoti kwamba kutumia machapisho hayo kumekuwa na matokeo sana, kwa sababu, jamii ya Waafrika ina desturi ya kujifunza kupitia hadithi badala ya mazungumzo yanayohusisha maswali na majibu. Mtu mwenye elimu anaweza kukubali kwa urahisi kusoma na kujifunza kwa njia ya maswali na majibu, lakini huenda haitafaa kutumia njia hiyo kwa mtu aliye na elimu ndogo. Ikiwa mwanafunzi anaweza kusoma kwa kiasi fulani, wahubiri wengi hupendelea kuanza kujifunza naye broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!, au Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!, au labda Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.

3. Kwa nini tunahitaji utambuzi ili tuweze kuwafundisha kwa njia yenye matokeo watu wenye tatizo la kusoma?

3 Wapongeze: Huenda wale ambao hawajajifunza kusoma wakaona haya, na wengi wanajiona kuwa hawafai. Mara nyingi, hatua ya kwanza ya kuwasaidia wajifunze ukweli ni kuwafanya wastarehe. Watu wengi wasioweza kusoma wana uwezo wa kushika mambo haraka na wanaweza kujifunza. Waheshimu na uwatendee kwa staha. (1 Pet. 3:15) Watachochewa kuendelea kujifunza ikiwa watahisi kwamba jitihada zao zinathaminiwa na wanafanya maendeleo ya kiroho. Usiache kuwapongeza.

Huenda wale ambao hawajajifunza kusoma wakaona haya, na wengi huhisi hawafai. Hatua ya kwanza ya kuwasaidia wajifunze ukweli ni kuwafanya wastarehe

4. Tunaweza kufanya nini ili kuwachochea wenye uwezo mdogo wa kusoma wajitayarishe kwa ajili ya funzo?

4 Hata kama mwanafunzi ana uwezo mdogo wa kusoma, mtie moyo ajitayarishe kwa ajili ya funzo. Baadhi ya wahubiri huko Afrika Kusini huwatia moyo wanafunzi wao wa Biblia wawaombe watu wa familia au rafiki zao ambao wanaweza kusoma vizuri wawasaidie. Mhubiri fulani huko Uingereza huwatia moyo wanafunzi wake wajitayarishe kwa kuwapa kitabu chake ili wakitumie wanapojifunza mafungu machache. Njia hiyo huwawezesha wanafunzi hao waone jinsi ilivyo rahisi kupata jibu ambalo limechorewa mstari. Ndugu mmoja huko India huwatia moyo wanafunzi wake watazame na kuzitafakari picha za somo litakalofuata.

5. Tunawezaje kuonyesha subira tunapoongoza funzo la mtu mwenye tatizo la kusoma?

5 Uwe Mwenye Subira: Unapotumia machapisho yoyote, kazia mambo makuu ya somo, na umsaidie mwanafunzi wako ayaelewe vizuri. Mwanzoni, mazungumzo ya dakika 10 hadi 15 huenda yakafaa zaidi. Usijaribu kuzungumzia habari nyingi sana, huenda ikafaa zaidi kujifunza mafungu machache kila mnapojifunza. Uwe mwenye subira ikiwa mwanafunzi anasoma taratibu. Huenda akachochewa kuboresha uwezo wake wa kusoma kadiri anavyojifunza mengi zaidi kumhusu Yehova. Ili kumsaidia mwanafunzi kufanya hivyo, itafaa ikiwa utamwalika ahudhurie mikutano mara tu mnapoanza kujifunza.

6. Tutawasaidiaje wajifunze kusoma?

6 Ikiwa wanafunzi wa Biblia wanajifunza kusoma watafanya maendeleo ya kiroho haraka zaidi. (Zab. 1:1-3) Wahubiri wengi wamewasaidia wanafunzi wao kwa kutumia broshua Jitahidi Kusoma na Kuandika kwa dakika chache kila baada ya funzo. Ikiwa mwanafunzi anavunjika moyo, labda unaweza kumtia moyo kwa kumtajia maendeleo fulani ambayo tayari amefanya. Mhakikishie kwamba Yehova atabariki jitihada zake, na umtie moyo asali ili Yehova amsaidie. (Met. 16:3; 1 Yoh. 5:14, 15) Wahubiri fulani huko Uingereza huwatia moyo wanafunzi wao wawe na miradi wanayoweza kuitimiza na ambayo itawawezesha kufanya maendeleo. Kwa mfano, mwanzoni mwanafunzi anaweza kujifunza alfabeti hadi azifahamu vizuri, halafu ajifunze jinsi ya kutafuta na kusoma maandiko fulani, na hatimaye kusoma machapisho ya Biblia yaliyorahisishwa. Mara nyingi kuwasaidia watu kusoma hakuhusishi kuwafunza jinsi ya kusoma tu, bali pia, kunahusisha kuwachochea wapende kusoma.

7. Kwa nini hatupaswi kusita kuwahubiria wale wenye tatizo la kusoma?

7 Yehova hawadharau watu walio na elimu ndogo. (Ayu. 34:19) Yeye huchunguza moyo. (1 Nya. 28:9) Kwa hiyo, usisite kuwahubiria wale wenye tatizo la kusoma. Kuna machapisho mengi mazuri sana unayoweza kuyatumia kuanza kujifunza pamoja nao. Hatimaye, unaweza kuendelea kujifunza nao kitabu Biblia Inafundisha na kuwasaidia waelewe Maandiko vizuri zaidi.

Ikiwa mwenye nyumba hawezi kusoma, jaribu madokezo haya:

  • Anza kwa kutumia Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele, au chapisho lingine linalofaa.

  • Mheshimu na umtendee kwa staha na usiache kumpongeza.

  • Usijaribu kuzungumzia habari nyingi sana.

  • Msaidie aboreshe ustadi wake wa kusoma.

Anapoendelea kuthamini kweli na kukuza tamaa ya kutaka kujifunza mengi zaidi, unaweza kuendelea kujifunza naye kitabu Biblia Inafundisha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki