Shiriki “Mambo Mema” kwa Kuwa Mkaribishaji-Wageni (Mt. 12:35a)
Bila shaka sote tunapenda kushiriki “mambo mema” pamoja na wengine kwa kufuata “mwendo wa ukaribishaji-wageni.” (Rom. 12:13) Wazee wameagizwa wawe kielelezo katika jambo hilo kwa kulipia gharama za usafiri na kuwaandalia chakula wasemaji wanaozuru. Hata hivyo, huenda tukawa na wasiwasi kuwakaribisha wageni nyumbani au tukasita kwa sababu hatuna uwezo mkubwa. Kufuata shauri ambalo Yesu alimpa Martha kutatusaidia kushinda hisia hizo. (Luka 10:39-42) Yesu alikazia kwamba “fungu jema” la ukaribishaji wageni ni ushirika na kitia moyo, wala si mlo wa pekee au nyumba yenye vitu vizuri. Kwa kutumia shauri hilo, sote tunaweza kushiriki “mambo mema” pamoja na ndugu zetu kama Neno la Mungu linavyosema.—3 Yoh. 5-8.