Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 29
JUMA LINALOANZA DESEMBA 29
Wimbo 37 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 18 ¶1-8 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoshua 12-15 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Toa “mambo mema” kutoka katika hazina njema tuliyokabidhiwa.—Mt. 12:35a.
Dak. 20: Wafundishe Wanafunzi wa Biblia na Watoto Wanaoamini “Mambo Mema,” Hatua kwa Hatua. (Mt. 12:35a) Mazungumzo. Eleza kile tunachopaswa kutarajia kutoka kwa wanafunzi wa Biblia na watoto wanaoamini, kwa kutumia maandiko yafuatayo: 1 Wakorintho 13:11; 1 Petro 2:2, 3. Fafanua maana ya ‘kuonja maziwa ya lile neno’ na ueleze jinsi tunavyoweza kuwasaidia wanafunzi na watoto wetu kufanya hivyo. Fafanua kanuni iliyo kwenye Marko 4:28. (Ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 2014, uku. 12, fu. 6-8.) Mhoji mzazi au mhubiri mwenye uzoefu kuhusu jinsi alivyomsaidia mtoto au mwanafunzi wa Biblia kufanya maendeleo ya kiroho.—Efe. 4:13-15; ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2014.
Dak. 10: “Shiriki ‘Mambo Mema’ Kwa Kuwa Mkaribishaji-Wageni (Mt. 12:35a).” Mazungumzo. Wengine wamenufaikaje au wamejionea mambo gani kwa kuwa wakaribishaji-wageni? Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi tunavyoweza kuwa wakaribishaji-wageni, hasa kuelekea wale walio katika utumishi wa wakati wote. Taja mipango ya kutaniko lenu ya kuwaandalia chakula wasemaji wanaozuru.
Wimbo 124 na Sala