Matayarisho Ni Muhimu Ili Kufundisha kwa Ustadi
Yesu aliulizwa swali kuhusu uzima wa milele katika pindi mbili tofauti, lakini alijibu kulingana na uhitaji wa aliyeuliza swali. (Luka 10:25-28; 18:18-20) Kwa hiyo, hata ikiwa tunaifahamu vizuri habari tutakayojifunza, tunahitaji kutayarisha kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi. Je, kuna jambo ambalo hataelewa au kukubali kwa urahisi? Ni maandiko gani tutasoma pamoja naye? Tutajifunza habari nyingi kadiri gani? Huenda tukahitaji kutayarisha mfano, maelezo, au maswali kadhaa yatakayomwezesha mwanafunzi kuelewa habari tutakayozungumzia. Kwa kuongezea, kwa kuwa Yehova ndiye anayeikuza mbegu ya kweli moyoni, tunapaswa kusali ili tupate mwongozo tunapojitayarisha kwa ajili ya funzo. Pia, tumwombe Yehova amsaidie mwanafunzi na abariki jitihada zetu za kumsaidia mwanafunzi huyo afanye maendeleo ya kiroho.—1 Kor. 3:6; Yak. 1:5..