Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/15 uku. 1
  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Habakuki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Habakuki
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Mtumaini Yehova Uishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Wenye Shangwe Katika Mungu wa Wokovu Wetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kitabu Cha Biblia Namba 35—Habakuki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Waovu Wataendelea Hata Lini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 12/15 uku. 1

Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Habakuki

1. Ni kwa njia gani hali yetu ni kama ya Habakuki?

1 Kadiri tunavyoona uovu unaongezeka ulimwenguni, huenda tukahisi kama Habakuki ambaye alimwuliza Yehova hivi: “Kwa nini unanionyesha jambo lenye kudhuru, nawe unaendelea kutazama taabu tupu?” (Hab. 1:3; 2 Tim. 3:1, 13) Kutafakari ujumbe wa Habakuki na kielelezo chake cha uaminifu kunatusaidia tunapotazamia siku ya hukumu ya Yehova.—2 Pet. 3:7.

2. Maisha yetu yanawezaje kuthibitisha kwamba sisi ni waaminifu?

2 Kuishi kwa Uaminifu: Badala ya kulemewa na hali mbaya alizokuwa akikabili, Habakuki aliendelea kuwa mwenye bidii na kubaki macho kiroho. (Hab. 2:1) Yehova alimhakikishia nabii huyo kwamba neno Lake lingetimizwa kwa wakati kabisa na kwamba “mwadilifu ataendelea kuishi kwa uaminifu wake.” (Hab. 2:2-4) Wakristo wanaoishi katika siku za mwisho wanajifunza nini? Jambo muhimu zaidi si kujua tu mwisho utafika lini bali ni kuwa na uhakika kwamba bila shaka utafika! Imani hutusaidia kubaki macho na kutanguliza utumishi.—Ebr. 10:38, 39.

3. Kwa nini tunapaswa kudumisha shangwe yetu tunapomtumikia Yehova?

3 Shangilia Katika Yehova: Gogu wa Magogu atakapowavamia watu wa Yehova, imani yetu itajaribiwa. (Eze. 38:2, 10-12) Hata washindi katika vita huwa wanakabili hali ngumu. Huenda kukawa na uhaba wa chakula, watu wakapoteza mali yao na hali ya maisha inaweza kuzorota. Tutatendaje chini ya hali hizo? Habakuki alitarajia hali ngumu, kwa hiyo aliazimia kudumisha shangwe yake alipomtumikia Yehova. (Hab. 3:16-19) Pia, “shangwe ya Yehova” itatusaidia kuvumilia majaribu ya wakati ujao.—Neh. 8:10; Ebr. 12:2.

4. Tunaweza kupata shangwe gani sasa na wakati ujao?

4 Wale ambao Yehova atawaokoa katika siku yake ya hukumu wataendelea kufundishwa jinsi Mungu anavyotaka tuishi. (Hab. 2:14) Watakaofufuliwa pia watajifunza kumhusu Yehova. Kwa hiyo, tutumie kila nafasi kumsifu Yehova na kutangaza kazi zake za ajabu!—Zab. 34:1; 71:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki