HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 52-59
“Mtupie Yehova Mzigo Wako”
Daudi alikabili majaribu mengi maishani mwake. Kufikia wakati ambapo Zaburi ya 55 ilitungwa, alikuwa amekabili mambo kama vile . . .
Matukano
Mateso
Hatia Kubwa
Msiba Katika Familia
Ugonjwa
Usaliti
Hata wakati ambapo mizigo yake ilikuwa mizito sana, Daudi alipata njia ya kukabiliana nayo. Alitoa shauri hili lililoongozwa na roho ya Mungu kwa mtu yeyote anayekabili hali kama yake: “Mtupie Yehova mzigo wako.”
Tunaweza kutumia mstari huo katika njia zipi leo?
Sali kwa Yehova kutoka moyoni unapokuwa na tatizo, wasiwasi, au jambo linalokuhangaisha
Tegemea Neno la Yehova na tengenezo lake likuongoze na kukusaidia
Fanya yote uwezayo kurekebisha hali kupatana na kanuni za Biblia