HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 60-68
Msifu Yehova, Msikiaji wa Sala
Sali kuhusu ahadi ulizomtolea Yehova
Kusali kuhusu ahadi zetu kutaimarisha azimio letu la kuzitimiza
Kujiweka wakfu kwa Mungu ndiyo ahadi ya maana zaidi tunayoweza kutoa
Hana
Onyesha unamtegemea Yehova kwa kummiminia moyo wako katika sala
Sala iliyojaa maana inapaswa kuhusisha hisia zetu za ndani sana
Tunapotoa sala hususa, tutaweza kutambua Yehova anapojibu sala hizo
Yesu
Yehova ni Msikiaji wa sala za watu wote wenye mioyo minyoofu
Yehova husikiliza sala za “watu wote wenye mwili” wanaotaka kumjua kikweli na wanaotaka kufanya mapenzi yake
Tunaweza kusali kwa Yehova wakati wowote
Kornelio
Andika mambo fulani unayotaka kutaja katika sala zako.