HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 87-91
Kaa Mahali pa Siri pa Aliye Juu Zaidi
Tunapata ulinzi wa kiroho katika “mahali pa siri” pa Yehova
Leo, ili tukae katika “mahali pa siri” pa Yehova ni lazima tujiweke wakfu na kubatizwa
Mahali hapo pa siri hapatambuliwi na wale ambao hawamtegemei Mungu
Wale walio mahali pa siri pa Yehova hawaathiriwi na mtu yeyote au kitu chochote kinachoweza kuhatarisha imani na upendo wao kwa Mungu
“Mwindaji wa ndege” anajaribu kutunasa
Ndege ni viumbe wanaojihadhari sana na wasionaswa kwa urahisi
Wawindaji huchunguza tabia za ndege kwa uangalifu na kisha kutafuta njia za kuwanasa
Shetani, “mwindaji wa ndege,” huwachunguza watu wa Yehova na kuweka mitego iliyokusudiwa kuharibu uhusiano wao na Yehova
Mitego minne hatari inayotumiwa na Shetani:
Kuwaogopa Wanadamu
Kupenda Vitu vya Kimwili
Burudani Zisizofaa
Tofauti za Kibinafsi