Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Septemba uku. 3
  • ‘Tembea Katika Sheria ya Yehova’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Tembea Katika Sheria ya Yehova’
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Habari Zinazolingana
  • Tegemea Neno la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Furaha Ujapokuwa Ulimwengu Wenye Kuvunja Sheria, Usio na Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Acha Neno la Mungu Liangaze Barabara Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Makumbusha na Maagizo ya Mungu wa Mfumo Mpya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
mwb16 Septemba uku. 3

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 119

‘Tembea Katika Sheria ya Yehova’

Kutembea katika sheria ya Yehova kunamaanisha kukubali kwa hiari mwongozo wa Mungu. Tuna mifano mingi mizuri katika Biblia ya wale ambao, kama mtunga-zaburi, walitii sheria ya Yehova na kumtegemea.

Mtunga-zaburi anatembea akiwa ameshika fimbo

Ili tuwe na furaha ya kweli, tunahitaji kutembea katika sheria ya Mungu

119:1-8

Yoshua akisoma kitabu cha kukunjwa

Yoshua alionyesha kwamba alikuwa na uhakika kamili katika mwongozo wa Yehova. Alijua kwamba ili kupata furaha na mafanikio ya kweli, alihitaji kumtegemea Yehova kwa moyo wake wote

Neno la Mungu hutupa ujasiri tunaohitaji ili kukabiliana na majaribu maishani

119:33-40

Yeremia akisali

Yeremia alionyesha ujasiri na alimtegemea Yehova alipokabili hali ngumu. Alidumisha maisha rahisi na alivumilia katika mgawo wake

Ujuzi sahihi wa Neno la Mungu hutupa uhakika wa kuhubiri

119:41-48

Paulo akimhubiria Gavana Feliksi

Paulo hakuogopa kuhubiri ujumbe wa Mungu kwa mtu yeyote. Alikuwa na uhakika kamili wa msaada wa Yehova alipomhubiria kwa ujasiri Gavana Feliksi

Mtunga-zaburi anatembea akiwa ameshika fimbo

Kati ya sehemu zilizoorodheshwa, ni wapi ninaweza kuonyesha uhakika zaidi ninapowahubiria wengine?

  • Shuleni

  • Kazini

  • Katika familia

  • Nyingine

Zaburi ya 119 imepangwa kialfabeti (au kiakrosti). Huenda mpangilio huo ulimsaidia mtunga-zaburi kuikumbuka. Zaburi hiyo ina beti 22, na kila ubeti una mistari 8. Kila mstari katika ubeti unaanza na herufi ileile ya alfabeti ya Kiebrania. Kwa kuwa alfabeti ya Kiebrania ina herufi 22, zaburi hiyo ina mistari 176, na hivyo hiyo ndiyo zaburi ndefu zaidi katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki