Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Novemba uku. 5
  • Jinsi ya Kutumia Kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutumia Kitabu Biblia Inatufundisha Nini?
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Habari Zinazolingana
  • Mwige Mwalimu Mkuu Unapotumia Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Wasaidie Wengine Watii Mambo Ambayo Biblia Inafundisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Biblia Inafundisha—Kitabu Chetu Kikuu cha Kufundishia Biblia
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
mwb16 Novemba uku. 5

MAISHA YA MKRISTO

Jinsi ya Kutumia Kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

Biblia Inatufundisha Nini?

Kitabu Biblia Inatufundisha kinafanana na kitabu Biblia Inafundisha. Vifaa hivyo vya kufundishia vinazungumzia kweli zilezile, kwa mpangilio uleule. Hata hivyo, kitabu Biblia Inatufundisha kinazungumzia mambo kwa njia rahisi zaidi na kinatumia maneno rahisi zaidi. Kimetayarishwa kwa ajili ya watu ambao wanashindwa kukielewa kitabu Biblia Inafundisha. Badala ya kuwa na nyongeza, kitabu Biblia Inatufundisha kina maelezo ya ziada yanayotoa ufafanuzi wa baadhi ya maneno na maelezo yanayozungumziwa katika sura mbalimbali. Sura hazina maswali ya utangulizi wala sanduku la pitio. Badala yake kuna muhtasari wa kweli za Biblia zinazofafanuliwa katika kila sura. Kitabu Biblia Inatufundisha kinaweza kutolewa wakati wowote hata ikiwa si toleo la mwezi, kama tunavyofanya na kitabu Biblia Inafundisha. Tunawezaje kutumia sehemu hizo za pekee za kitabu Biblia Inatufundisha tunapoongoza funzo la Biblia?

Muhtasari wa sura katika kitabu Biblia Inatufundisha

MUHTASARI: Kwa watu wengi, njia yetu ya kawaida ya kuongoza funzo la Biblia kwa kusoma fungu na kisha kuuliza swali inafaa tunapotumia kitabu Biblia Inafundisha. Lakini namna gani ikiwa mwanafunzi haelewi vizuri lugha au hawezi kusoma vizuri? Katika visa kama hivyo unaweza kuamua kutumia kitabu Biblia Inatufundisha. Kisha, muhtasari wa sura unaweza kutumiwa kama msingi wa funzo na mwanafunzi anaweza kutiwa-moyo ajisomee mafungu katika sura hiyo kwa wakati wake mwenyewe. Kila kweli ya Biblia inaweza kufundishwa katika kipindi cha dakika 15 hivi. Kwa kuwa muhtasari hauna habari zote zinazopatikana katika mafungu, mwalimu anahitaji kujitayarisha vizuri, na kufikiria kwa makini mahitaji ya mwanafunzi. Ikiwa ataongoza funzo kwa kutumia njia ya kawaida ya kusoma mafungu, basi muhtasari unaweza kutumiwa kama pitio.

Maelezo ya ziada katika kitabu Biblia Inatufundisha

MAELEZO YA ZIADA: Maelezo ya ziada yameorodheshwa kwa kutegemea mahali ambapo maneno hayo yalizungumziwa kwa mara ya kwanza katika kitabu. Mwalimu anaweza kuamua ikiwa atazungumzia maelezo ya ziada katika kitabu Biblia Inatufundisha wakati wa funzo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki