MAISHA YA MKRISTO
Kutunza Maeneo Yetu ya Ibada
Majumba yetu ya Ufalme si majengo tu; ni maeneo ya ibada yaliyowekwa wakfu kwa Yehova. Kila mmoja wetu anaweza kufanya nini ili kushiriki kutunza Jumba la Ufalme? Zungumzieni maswali yafuatayo baada ya kutazama video Kutunza Maeneo Yetu ya Ibada.
Majumba ya Ufalme yanatimiza kusudi gani?
Kwa nini tunapaswa kudumisha Jumba la Ufalme likiwa safi na katika hali nzuri?
Ni nani anayepaswa kudumisha Jumba la Ufalme?
Kwa nini usalama ni muhimu, na ni mifano gani ya kudumisha usalama uliyoona katika video?
Tunaweza kumwonyeshaje Yehova heshima kwa michango yetu?