Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Juni uku. 8
  • Furahia Kuhubiri Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Furahia Kuhubiri Habari Njema
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Habari Njema Hizi za Ufalme Tuzihubiri
    Mwimbieni Yehova Sifa
  • Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • ‘Kuleta Habari Njema za Jambo Bora’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Juni uku. 8

MAISHA YA MKRISTO

Furahia Kuhubiri Habari Njema

Je, umewahi kuhisi ni vigumu kuhubiri? Wengi wetu wangejibu ndiyo. Kwa nini? Labda tunakutana na watu wasiopendezwa au wenye uhasama au tunaogopa kuzungumza na watu tusiowajua. Mambo hayo yanaweza kutufanya tupoteze shangwe yetu. Hata hivyo, tunamwabudu Mungu mwenye furaha ambaye anataka tumtumikie kwa kushangilia. (Zb 100:2; 1Ti 1:11) Ni sababu gani tatu zinazotufanya tufurahie kuhubiri?

Kwanza, tunatangaza ujumbe wa tumaini. Watu wengi leo hawana tumaini, lakini tunaweza kuwapa “habari njema za jambo bora.” (Isa 52:7) Isitoshe, habari njema ya Ufalme wa Mungu inaweza kutujaza shangwe sisi wenyewe pia. Kabla ya kwenda kuhubiri, tafakari kuhusu baraka ambazo Ufalme wa Mungu utaleta duniani.

Pili, habari njema tunayohubiri inawafaidi watu kimwili na kiroho. Wanajifunza kuacha mazoea mabaya na kuwa na tumaini la kupata uzima wa milele. (Isa 48:17, 18; Rom 1:16) Tunaweza kuwazia tunafanya kazi ya kuwatafuta na kuwaokoa watu. Hata ikiwa watu fulani hawataki kuokolewa, bado tunaendelea kuwatafuta wale wanaotaka kuokolewa.—Mt 10:11-14.

Sababu ya tatu na muhimu zaidi ni kwamba kazi yetu ya kuhubiri inamletea Yehova heshima. Anathamini sana kazi yetu ya kutoa ushahidi. (Isa 43:10; Ebr 6:10) Zaidi ya hilo, anatupatia kwa ukarimu roho yake takatifu ili tutimize kazi hiyo. Kwa hiyo, msihi Yehova akupe shangwe, tunda la roho takatifu. (Ga 5:22) Kwa msaada wake, tunaweza kushinda mahangaiko yetu na kuhubiri kwa ujasiri. (Mdo 4:31) Hivyo, hata itikio liweje katika eneo letu, tutafurahia mgawo wetu wa kuhubiri.—Eze 3:3.

Mtazamo unaotofautiana kuhusu kazi ya kuhubiri​—mmoja hana furaha mwingine ana shangwe

Ungependa kuwa na mtazamo gani katika huduma? Unaweza kuonyeshaje kwamba una shangwe?

TAZAMENI VIDEO PATA SHANGWE TENA KWA KUJIFUNZA NA KUTAFAKARI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini tunapaswa kuwa na mazoea mazuri ya kujilisha kiroho hata ikiwa tunahubiri saa nyingi kila mwezi?

  • Tunahitaji kumwiga Maria katika njia gani?

  • Wewe unatenga wakati lini ili kutafakari Neno la Mungu?

  • Unapohubiri habari njema, ni nini kinachokufanya uwe na furaha?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki